Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA INA KIKOSI CHA KAWAIDA SANA, SAJILINI

Na Prince Hoza Matua

TIMU ya Azam FC imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba SC usiku wa jana Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, beki wa kati Lameck Elias Lawi dakika ya 73 na sasa Azam FC itakutana na mshindi wa Nusu Fainali ya pili hii leo kati ya Yanga SC na Singida Black Stars.

Huo ni ushindi wa pili kwa Azam FC dhidi ya Simba SC katika mechi zilizochezwa karibuni, kwani Desemba mwaka jana Azam FC iliifunga Simba mabao 2-0 katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu bara inayodhaminiwa na benki ya NBC ambao ni wadhamini wa kombe la Mapinduzi.

Lakini pia ni ushindi wa pili mfululizo wa kocha Florent Ibenge raia wa DR Congo ambaye tangu alipopewa jukumu la kuinoa Azam FC akitokea Al Hilal Omduman ya Sudan, amekuwa mwiba mchungu kwa Simba.

Katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu bara dhidi ya Azam FC, Simba ilikuwa inanolewa na meneja mkuu Dimitar Pantev raia wa Burgalia, na baada ya mchezo huo uongozi wa Simba na meneja huyo waliamua kusitisha mkataba wao na jukumu hilo akaschiwa Seleman Matola ambaye ni kocha msaidizi.

Lakini kiukweli mwenendo wa Simba ndani ya misimu minne sasa sio mzuri, licha kwamba msimu uliopita klabu ilipata mafanikio makubwa ya kufanikiwa kucheza fainali ya kombe la Shirikisho Afrika, ila mimi nasema ukweli mwenendo wa Simba si mzuri.

Simba ilikuwa inanolewa na Fadlu David's raia wa Afrika Kusini ambaye aliifanya timu hiyo icheze fainali, lakini nilivyoitazama kiundani nikaona sio nzuri kiushindani.

Kombe la Shirikisho Afrika ni shindano dogo na linaloshirikisha timu ndogo tofauti na Ligi ya mabingwa barani Afrika, na ndio maana hata timu za madaraja ya chini zinapata nafasi ya kushiriki michuano hiyo.

Kundi ambalo walipangwa Simba lilikuwa dhaifu na ndio maana ilitoboa kiwepesi, lakini ilikutana na ushindani mkubwa kwenye ligi ya ndani pale ilipokutana na washindani wake wakuu Yanga na Azam ambapo Simba ilishindwa kuondoka na pointi ya ushindi na kujikuta ikiukosa ubingwa wa bara.

Tatizo kubwa la Simba tangu chini ya Fadlu ni kukosa wachezaji bora wanaoweza kuamua mechi kubwa, Simba imekuwa na tatizo na imekuwa ikikosa mtu wa kusimama kidete na kuishika timu pinzani kwenye mchezo ambao Simba inatakiwa kushinda.

Ushindani wa ndani, Simba inaonekana kuzidiwa pindi inapokutana na Yanga, Azam na hata Simba, malalamiko yao makubwa kwa mashabiki wake pindi ikishindwa kupata matokeo, wanayopeleka kwa kocha msaidizi Seleman Matola wakisema anawahujumu.

Lakini pia shutumu wanazipeleka kwa mwenyekiti wao wa klabu Murtaza Mangungu, kiukweli hao wote wanaowalalamikia mashabiki sio wahusika wanaosababisha timu isifanye vizuri.

Wapo baadhi ya wanachama wa klabu hiyo wamegeukia ushirikina na wakaenda kwa Masheikh kushitakiwa kufanya kwao vibaya na kusoma albadiri Ili kusudi kumdhuru anayetajwa kuwa na muharibifu kwa timu yao.

Lakini ukweli ni kwamba Simba inatakiwa kufanya usajili wa wachezaji wenye quality kubwa na ikiwezekana waizidi Yanga na kutawala soka la Tanzania, Simba inatakiwa irudi kwenye njia yake kuu, itwae ubingwa wa bara, kombe la CRDB na Ngao ya Jamii, lakini ioneshe ushindani ngazi ya kimataifa hasa Ligi ya mabingwa.

ALAMSIKI





 


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...