Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais wa FIFA alaani vikali vurugu za AFCON Morocco

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulimwenguni (FIFA),
Gianni Infantino, amelaani vikali matukio ya utovu wa nidhamu yaliyotokea katika mchezo wa fainali nchini Morocco, akisisitiza kuwa vitendo vya vurugu na uamuzi wa kuacha uwanja havikubaliki.
Katika taarifa yake aliyoituma kwa AFP, Infantino alisema:

"Tunalaani vikali tabia ya baadhi ya 'mashabiki' pamoja na baadhi ya wachezaji wa Senegal na wafanyakazi wa kiufundi.

Haikubaliki kuacha uwanja wa michezo kwa njia hii, na vile vile, vurugu haziwezi kuvumiliwa katika mchezo wetu, si sawa kabisa."

Rais huyo alitumia fursa hiyo kuipongeza Morocco kwa uandaaji mzuri, akitaja kuwa ni maandalizi tosha kwa taifa hilo kuelekea kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia la mwaka 2030.

Kwa upande mwingine, kocha wa Morocco, Walid Regragui, alielezea kusikitishwa kwake na taswira mbaya ambayo soka la Afrika limeionyesha mbele ya macho ya ulimwengu kutokana na fainali hiyo iliyotawaliwa na machafuko. Regragui alibainisha kuwa uharibifu huo wa sifa ni mkubwa na kuongeza: "

Taswira tuliyotoa kuhusu soka la Afrika ilikuwa ya aibu sana. Kulazimika kusimamisha mchezo kwa zaidi ya dakika 10 huku ulimwengu ukiutazama si jambo la kawaida sana."

Kauli yake inaakisi hofu ya wadau wengi wa soka barani humu juu ya jinsi matukio kama hayo yanavyoweza kurudisha nyuma juhudi za kukuza hadhi ya mchezo huu kimataifa.

Kufuatia sakata hilo, Tume ya Nidhamu ya CAF inatarajiwa kutoa adhabu kali na ya muda mrefu dhidi ya kocha wa Senegal, Pape Thiaw, kwa kuhusika na uamuzi wa kuiondoa timu uwanjani (kutoa timu).

Hatua hii inakuja wakati Rais wa CAF, Dr. Patrice Motsepe, akiwa na msimamo thabiti wa kuhakikisha nidhamu inatawala ili kulinda heshima ya bara hili, akisisitiza kuwa "Tunaendesha Afrika kwa ajili ya Waafrika."

Ingawa idadi kamili ya mechi atakazofungiwa Thiaw bado haijawekwa wazi, adhabu hiyo inatazamwa kama fundisho kwa makocha na viongozi wengine wanaojihusisha na migomo ya aina hiyo uwanjani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...