Ruka hadi kwenye maudhui makuu

GAMONDI APEWE MKATABA WA KUDUMU KUNOA STARS YA AFCON 2027

Na Prince Hoza Matua

NAWATAKIA kheri ya mwaka mpya wa 2026 na pia nawapa pole wale wote ambao walipoteza ndugu zao mwaka jana, lakini wengine wameuona mwaka mpya ila hawapo sawa kiafya, mwenyezi Mungu awape uzima na kurejea kwenye utimamu wa afya kusudi tulijenge vema taifa hili la Tanzania na dunia kwa ujumla.

Bila shaka Watanzania tumeingia mwaka mpya wa 2026 tukiwa na furaha tele kufuatia timu yetu ya taifa, Taifa Stars kufuzu hatua ya 16 bora ya AFCON inayofanyika nchini Morocco.

Shukrani kubwa ziwaendee wachezaji, benchi la ufundi la timu hiyo na viongozi wa Shirikisho la soka nchini, TFF kwa kufanikisha timu hiyo inaandika rekodi ya mara ya kwanza kufika hatua hiyo.

Lakini kubwa ni kwa kaimu kocha mkuu wa timu hiyo Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina ambaye uwepo wapo umesaidia timu hiyo kufika hapo, nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitawapongeza makocha wengine waliofanya vizuri aliwemo Hemed Morocco ambaye alikuwa kocha mkuu wa timu hiyo.

Morocco akisaidiana na Juma Mgunda na Jamhuri Kihwelu Julio walisaidia timu hiyo kufuzu fainali za AFCON za mwaka 2025 zinazoendelea Morocco, hivyo ba wao huenda leo hii tusingezungumza chochote kuhusu Taifa Stars.

Miguel Gamondi alipewa jukumu la kuinoa Taifa Stars kama kaimu kocha akichukua mikoba ya Hemed Suleiman Morocco na moja kwa moja aliingiza timu kambini kujiandaa na AFCON.

Wengi tuliona kama miujiza kumpa Gamondi timu hiyo zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kuanza kwa fainali zenyewe, kwani muda wa maandalizi haukutosha kabisa, pia Gamondi alikuwa na kibarua kingine cha kuinoa klabu ya Singida Black Stars akiwa kama kocha mkuu.

Ikumbukwe Singida Black Stars ipo katika michuano ya kombe la Shirikisho Afrika na ikiwa imetinga makundi hivyo itakuwa ngumu kwa kocha huyo kujigawa kwenye majukumu mawili.

Kwa kifupi wengi tulijua kwamba Stars inakwenda kupiga maktaimu au kushiriki kwa mara nyingine, hakuna hata Mtanzania mmoja aliyeipa nafasi ya kusonga mbele timu hiyo, lakini pia hofu ilitanda wakiamini kwamba Gamondi hawezi kufika mbali kutokana na kundi ambalo imepangwa Taifa Stars ni gumu.

Taifa Stars ilipangwa kundi C na timu ngumu za Nigeria, Tunisia na Uganda ambazo zote zimekuwa tishio kwa Tanzania, nafasi ya mwisho iliandaliwa Stars na hata aliyekuwa kocha msaidizi wa timu hiyo Jamhuri Kihwelu Julio alisikika akibeza kuachwa kwao na kumpa Gamondi.

Julio aliamini kwamba Gamondi kama ni kocha bora zaidi yao basi awafilishe nusu fainali jambo ambalo ni kumbeza ingawa lolote linaweza kutokea kwenye soka, baada ya kuiwezesha timu hiyo kutinga hatua ya 16 bora AFCON, TFF sasa wanatakiwa kumuandalia mkataba wa kudumu.

Gamondi anapaswa kupewa mkataba wa kudumu kwa sababu ya jukumu kubwa lililo mbele ambalo yeye pekee anaweza kututoa kimasomaso, mwaka 2027 Tanzania itakuwa mwenyeji mwenza wa michuano ya AFCON hivyo ni bora tuanze maandalizi mapema.

Ushiriki wa Tanzania katika fainali za AFCON za mwaka 2025 nchini Morocco zilikuwa nzuri na tumepiga hatua hivyo michuano ijayo tuweke historia zaidi ikiwezekana tufike robo fainali au fainali yenyewe.

Kwa Gamondi inawezekana, kwani ni miongoni ya makocha ambao wanajitambua, kitendo cha kuibana Nigeria na Tunisia vilitosha kabisa kudhihirisha kwamba Stars ya Gamondi imefanya makubwa.

Kila la kheri wapenzi na wasomaji wa ukurasa wangu wa Mambo Uwanjani Blog.
ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...