Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AISHI MANULA ANARUDI GOLINI NA KUWA TANZANIA ONE AU ANAITAFUTA NAMBA AZAM FC?

Na Prince Hoza Matua

MICHUANO ya kombe la NMB Mapinduzi Cup imemalizika siku ya Jumanne iliyopita ambapo miamba Yanga SC na Azam FC zilicheza fainali katika uwanja wa Gombani mjini Pemba.

Yanga SC waliibuka mabingwa wa michuano hiyo kufuatia mikwaju ya penalti 5-3 baada ya sare 0-0 ndani ya dakika 120, golikipa wa Azam FC, Aishi Salum Manula alitokea kuwa gumzo katika mchezo huo baada ya kufanikiwa kuzuia penalti.

Kipa huyo wa zamani wa Simba SC, alizuia penalti iliyopigwa na kiungo mshambuliaji wa Yanga, Pacome Zouzoua, hata hivyo Manula amekuwa bora katika michuano hiyo kuanzia mchezo wake wa kwanza na mpaka wa mwisho.

Manula amekuwa bora kiasi kwamba watazamaji hawaamini alichonacho, Manula ni zao la Azam FC, kwani Simba SC walimchukua mikononi kwa Azam FC aliyejiunga nayo akitokea Mtibwa Sugar ya Manungu mkoani Morogoro.

Ikumbukwe Manula akiwa Azam FC, alikuwa kipa chaguo la kwanza lakini alikutana na changamoto kadhaa mpaka kumfanya awe kipa wa kwanza kwenye timu hiyo.

Manula alijizolea sifa kemkem kiasi kwamba akabeba Mataji mbalimbali ikiwemo ubingwa wa Ligi Kuu bara, kombe la Mapinduzi na baadaye Klabu Bingwa Afrika mashariki na kati, maarufu kombe la Kagame Cup.

Simba walipoona hawapati mafanikio kwa muda mrefu wakaamua kuvamia Chamazi na kuwakomba nyota wanne wa Azam FC na kuwachukua, nyota hao ni Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, John Bocco na Manula.

Ilikuwa msimu wa 2016/2017 na Simba ilifanikiwa kurejesha ubingwa wa bara, na baada ya hapo Simba ikiwa bingwa wa bara mfululizo na makombe mengine ikiwemo Ngao ya Jamii, Manula aliendelea kuwa kipa chaguo la kwanza ndani ya klabu yake ya Simba na timu ya taifa, Taifa Stars.

Ingawa Tanzania ilijaaliwa makipa wengi bora, lakini umahiri wa Manula haukuwa na mfano wake, Manula alikuwa kipa bora kiasi kwamba bara la Afrika lilitokea kumkubali na kumfanya miongoni mwa makipa wa kipekee.

Bahati mbaya Manula aliandamwa na majeraha ya mara kwa mara, lakini jeraha kubwa lililompata hadi kupelekea nafasi yake ya kukaa golini ni lile la kutunguliwa mabao matano na watani wao Yanga.

Katika mchezo wa Ligi Kuu bara, Yanga iliifunga Simba mabao 5-1 ambapo goli la Simba kipa alikuwa Aishi Salum Manula, kipigo hicho hakitasahaulika kamwe kwani Wanasimba wanaamini kwamba kipa Manula alihujumu timu.

Na kuanzia hapo kipa huyo alipoteza namba yake ya kukaa golini, Simba ilifungwa na Yanga bao 5-1 msimu wa 2023/2024 na baada ya hapo Manula hakuonekana tena langoni.

Makocha wote wa Simba hawakumpa nafasi ya kukaa golini nadhani kimaelekezo toka kwa uongozi, na baada ya mkataba kwisha wakaachana naye, Manula akasajiliwa na Azam FC lakini akiwa tayari amepoteza namba ya kudumu.

Katika kikosi cha Azam FC, kocha wa timu hiyo anamtumia Zuberi Foba kama kipa chaguo la kwanza na Issa Fofana kipa chaguo la pili, na Aishi Manula ni kipa chaguo la tatu.

Katika michuano ya kombe la NMB Mapinduzi Cup, kocha Florent Ibenge raia wa DR Congo, amemtumia Manula kama kipa chaguo la kwanza na akafanikiwa kumdhihirisha kwamba yeye ni kipa bora, Manula amewaziba midomo waliomsakama na huenda nafasi yake ya kuwa Tanzania one ikarejea.

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...