Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simon Happygody Msuva; Mfungaji bora wa muda wote Taifa Stars


Bao lake dhidi ya Uganda kwenye AFCON 2025 ni la 21 akiwa na Taifa Stars, na kumfanya @smsuva27 kuwa mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.

Msuva ambaye ni zao la akademi ya @azamfcofficial, anampita Mbwana Samatta mwenye mabao 20.

Hapa nazungumzia mabao ya Taifa Stars tu. Mrisho Ngassa anatajwa kama mfungaji bora wa muda wote, lakini sio sahihi.

Kwa Taifa Stars, Ngassa ana mabao kumi tu, ambayo hayamfanyi hata kuwemo kwenye tano bora.

Katika kuhesabu haya mabao kuna kosa kubwa sana hufanyika. Watu huchanganya mabao ya Taifa Stars na ya Kilimanjaro Stars.

Taifa Stars ndio timu ya taifa ya Tanzania, ikijumuisha wachezaji kutoka bara na visiwani.

Hii ndio timu inayoshiriki AFCON, Kombe la Dunia na mechi rasmi za kimataifa.

Kwenye timu hii, Msuva amefunga mabao 21, na ndio anaongoza.

Samatta ana mabao 20, anafuata.

Ngassa ana manao 10.

Halafu Kilimanjaro Stars ni timu ya Bara, ambayo hushiriki CECAFA Senior Challenge Cup pekee.

Kwenye timu hii, Ngassa ana mabao 15, anaongoza. Msuva ana mabao manne na Samatta ana mabao mawili tu.

Kilimanjaro Stars wapinzani wake ni pamoja na Zanzibar. Haiwezekani mfungaji bora wa muda wote wa nchi halafu baadhi ya mabao yake kaifunga nchi hiyo hiyo...ndio hadithi ya Ngassa.

Katika mabao yake 15 ya Kilimanjaro Stars, moja kafunga dhidi ya Zanzibar, mwaka 2009, kwenye CECAFA iliyofanyika Kenya.

Tunapohesabu mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya Tanzania, tunaangalia mabao ambayo yamefungwa na Taifa Stars...sio Kilimanjaro Stars.

Na hapa ndipo Simon Msuva anapoongoza. Ngassa anabaki kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Kilimanjaro Stars.

Msuva anakuwa mfungaji bora wa muda wote kwa mabao ya ndani ya miaka 8 tu.

Bao lake la kwanza alifunga Machi 28, 2017 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Burundi.

Stars ilishinda 2-1, bao la pili lilifungwa na Mbaraka Yusuf...la Burundi lilifungwa na Mavugo!

Simon Msuva



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa