Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mrithi wa Manula bado hajapatikana Tanzania

Anaandika George Ambangile

Kila nikijitahidi kuamini kama zama za Aishi Manula zimekwisha kwenye soka la Tanzania moyo wangu unakua mzito kulipokea jambo hili naona kama ni mapema sana kwa sababu mbadala halisi wa kipa huyu bado hajapatikana.

Baada ya kufungwa mabao matano na Young Africans Sc ni kama Simba Sc waliamua kumgeuzia kisogo na kumtoa kwenye ramani ya soka kabisa Ila madhara makubwa yanatokea kwenye timu ya taifa ya Tanzania.

Naheshimu uteuzi wa makipa wanaoitwa timu ya taifa, lakini ule ukomavu, uzoefu na ubora alionao Aish Manula bado haujaanza kuonekana labda niseme ni papara au haraka zangu Ila hawa makipa walipaswa kujifunza zaidi mbele ya Manula.

Makipa wa sasa makosa yao yamekua mengi na tena ya kujirudia tunaenda Afcon nchini Morocco ni heri benchi la ufundi Kuliangalia jambo hili mapema japo naheshimu maamuzi yenu na timu ya taifa ni timu ya wachezaji wote.

Uganda waliamua kufanya maamuzi magumu kumrejesha Dennis Onyango timu ya taifa wanajua kabisa wanaenda kwenye mashindano ya Afcon na wanaona bado kuna mchango Onyango anaweza akautoa timu ya taifa.

Kipa mkomavu mzawa kama Manula ambaye amecheza mashindano makubwa kwa ngazi ya vilabu na timu ya taifa bado hayupo kumbuka kuna muda alikua anapunguza idadi kubwa ya magoli nan anakumbuka mechi ya Nigeria na Tanzania kule nchini Nigeria, Simba na Asec Memosas kule Ivory Coast kwa kupangua penati 2.

Jambo hili linaweza kutuumiza wenyewe wakati bado tuna nafasi ya kufanya maamuzi sahihi na kwanini waliamua kumuita Tanzania one wakati kuna makipa wengi kwenye ligi Yetu.

Kwa sasa hatuna kipa mzawa na mwenye upekee kama Aish Manula narudia tena ubora, ukomavu, uzoefu na uongozi wake kiwanjani ni unakosekana na unahitajika kwa kiasi kikubwa.

Nembo ya makipa wazawa kwa sasa tunaamua kuipoteza wenyewe muda bado upo wa kufanya maamuzi na umri wake bado unaruhusu.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa