Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MIGUEL GAMONDI ANAWEZA KUWA MWAROBAINI WA TAIFA STARS AFCON 2025

Na Prince Hoza Matua

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limemtambulisha Muargentina Miguel Angel Gamondi kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya wakubwa ‘Taifa Stars’ baada ya kuachana na mzawa, Hemed Suleiman Ali ‘Morocco’.
Gamondi ataiongoza Tanzania kwa mara ya kwanza katika mchezo wa kirafiki wa Kimataifa dhidi ya Kuwait Ijumaa ya Novemba 14 Uwanja wa Al Salam Jijini Cairo nchini Misri.

Ni wiki kocha huyo wa Singida Black Stars alipotangazwa kuwa kocha mpya wa Taifa Stars akichukua nafasi ya mzawa, Hemed Suleiman Ali ‘Morocco’ aliyeondolewa.

Gamondi amekitaja kikosi chake kwa ajili ya mchezo huo baada ya mechi za wikiendi za Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara tayari kwa safari ya Misri.

TFF imechukua hatua hiyo ya kumfuta kazi Morocco na kumwajiri Gamondi ambaye mafanikio yake akiwa na klabu ya Yanga SC pamoja na Singida Black Stars tunayafahamu.

Kocha huyo kipenzi cha wengi alijiunga na Yanga msimu juzi akichukua mikoba ya Nasreddine Nabi raia wa Tunisia ambaye naye aliiwezesha Yanga kufika fainali ya kombe la Shirikisho Afrika.

Baada ya Yanga kufika hatua hiyo ya fainali, Nabi aliamua kuachana na timu hiyo na kutimkia klabu ya FAR Rabat ya Morocco, mbali na kuwafikisha Yanga fainali ya kombe la Shirikisho Afrika, aliiwezesha kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu bara na kombe la FA huku pia ikibeba Ngao ya Jamii mwanzoni mwa msimu.

Alipoondoka Nabi, uongozi wa Yanga ulimtambulisha Muargentina huyo ambaye alikwenda kuibadili zaidi Yanga na kuwa miongoni mwa timu tishio barani Afrika, ikiwa na Gamondi Yanga iligeuka mbabe kwa mtani wake Simba, ikianza kwa kuifunga Simba mabao 5-1.

Gamondi akiwa na Yanga iliweza kuifunga Simba mara nne mfululizo kabla ya makocha wenzake wawili Miloud Hamdi raia wa Algeria na Ramon Folz raia wa Ufaransa kuendeleza vipigo kwa Simba na kuwa mara sita mfululizo.

Lakini pia Gamondi aliiwezesha Yanga kutetea mataji yake ya ndani yaani Ligi Kuu bara, kombe la FA na Ngao ya Jamii, vile vile Yanga ilifanikiwa kwa mara ya kwanza kutinga robo fainali ya michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika baada ya mwaka 1998.

Mpira wa Gamondi hakuna shabiki wa soka hapa nchini ambaye haujuwi, Yanga ya Gamondi ilikuwa inasifika kwa soka lake la kushambulia kwa kasi kiasi kwamba timu mbalimbali hasa zile zenye majina makubwa kama Mamelodi Sundown's ya Afrika Kusini au CR Belouizdad ya Algeria zilikutana na moto wake.

Yanga ya Gamondi iliogopeka mpaka pale alipoanza kuhujumiwa na baadaye akaondoka nchini, Singida Black Stars ilimrejesha tena Tanzania na kumpa jukumu la kuinoa timu yake ilianza kushiriki kombe la Klabu bingwa Afrika mashariki na kati, (Kagame Cup).

Kocha huyo aliiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa, na sasa ameiwezesha kutinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho Afrika, maamuzi ya TFF kumpa kibarua cha kuinoa Taifa Stars ambayo baadaye itakwenda kushiriki fainali za AFCON zitakazofanyika Morocco.

Nina imani na Gamondi kwenye fainali za AFCON na mashindano mengine ambapo Stars itakwenda kushiriki, Gamondi ni kocha wa misheni, hivyo tutegemee makubwa kutoka kwake, Stars ilihitaji kocha aina ya Gamondi muda mrefu isipokuwa mamlaka ilikuwa inapuuza maoni ya wadau.

Naishukuru TFF kwa kusikiliza maoni ya wadau wakianza na wale waliokuwa wanataka kocha Hemed Morocco afutwe kazi, Morocco hakupaswa kuendelea kuinoa timu hiyo kwani kwa ukubwa wa Stars ilihitaji kocha mwenye uwezo mkubwa.

Gamondi ni kocha wa misheni hivyo wachezaji sasa wanatakiwa kutimiza malengo, bilioni vya Watanzania kwa timu ya taifa vilikuwa kwa kocha ambaye alishindwa kuwaunganisha ndani ya uwanja, Gamondi anajua kuunganisha wachezaji na haitachukua muda mrefu timu yetu itapata mafanikio.

ALAMSIki




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa