Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Heri Mzozo aliomba laki 6 akapewa milioni 15 na Tshabalala

Meneja wa mchezaji wa Yanga SC Mohamed Hussein Zimbwe anayejulikana kwa jina la Carlos Mastermind amejibu malalamiko ya mlezi wa kisoka wa Mohamed Hussen anayejulikana  kwa jina la Heri Mzozo (Kheri Chibakasa).

Carlos amejibu baada ya awali Heri Mzozo kusikika katika vyombo vya habari akidai kuwa amewasaidia wachezaji wengi ila hakuna anayemjali baada ya kufanikiwa na wanaishi maisha mazuri ilihali yeye kapanga ameshindwa hadi kumalizia nyumba yake.

Carlos akihojiwa na Clouds alisema kuwa Mohamed Hussein amewahi kumpa Heri Mzozo milioni 15 amalizie nyumba yake baada ya awali kupiga simu kuomba laki sita za Kodi.

“Samahani kama nitakuwa namdhalilisha ila hii lazima niweke wazi kama shuhuda, mwaka juzi Heri alinipigia akaniambia mimi nadaiwa kodi laki sita, kesho yake nikampigia yeye pamoja na Tshabalala (Mohamed Hussein) ishu ikiwa kwa nini hadi sasa hivi ana shida ya kodi ya nyumba”

“Tukafika tukaongea na nikasema suluhu hapa sio kodi,leo Tshabalala anaitoa hii laki sita baada ya miezi mitatu itarudi tena, nikamwambia Heri wewe ukipata Tsh ngapi unamaliza nyumba yako? 

Akasema akipata milioni 20 anakamilisha kila kitu, nikamwambia Tshabalala hiyo laki sita mpe, halafu hiyo milioni 20 ya kumaliza nyumba yako nitakurudia,.

Baada ya siku saba Tshabalala akampa Heri milioni 15 kati ya 20 aliyohitaji, sasa ameongea kama Tshabalala hajawahi kumsaidia kabisa”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa