Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA NA FAINALI MBILI ZA CAF

Na Prince Hoza

NAWAPA hongera Wekundu wa Msimhazi, Simba SC kwa kufanikiwa kuingia fainali ya kwanza ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Simba imeingia fainali baada ya kuiondosha timu ya Stellanboch ya Afrika Kusini kwa jumla ya bao 1-0, ilipata ushindi jijini Dar es Salaam katika uwanja wa Mkapa, na mwishoni mwa wiki iliyopita ikilazimishwa sare tasa 0-0 uwanja wa Moses Mabhida jijini Durban nchini Afrika Kusini.

Hii ni fainali yake ya kwanza kwa Wekundu hao wa Msimhazi, lakini ni fainali yake ya pili katika historia ya klabu hiyo tangia ilipoanzishwa mwaka 1935, mwaka 1993 Simba iliingia fainali ya michuano ya kombe la CAF.

Shirikisho la soka barani Afrika lilikuwa na michuano yake mitatu ya ngazi ya vilabu, Klabu Bingwa Afrika ambapo mabingwa wa nchi husika barani humu hushiriki michuano hiyo, na kombe la Washindi ambapo wanaoshika nafasi ya pili nao hushiriki michuano hiyo.

Lakini Shirikisho hilo liliamua kuanzisha michuano mingine ambayo wanaoshika nafasi ya tatu nao hushiriki, lakini pia nchi zilianzisha michuano ya ndani ya vilabu kama kombe la FA ambapo Bingwa alipata nafasi ya kushiriki michuano mipya ambayo iliitwa kombe la CAF.

Na mwaka 1993 klabu ya Simba ya Tanzania ikiwa kwenye nafasi ya tatu kwenye Ligi ya nchi, ilipata nafasi ya kushiriki michuano hiyo, Wekundu hao walifanikiwa kufika fainali ambapo ilijikuta inakutana na mwakilishi wa Ivory Coast Stella Abdijan na kufungwa mabao 2-0 na kombe lilienda Ivory Coast.

Sitaki kuyakumbusha ya 1993 kwani yaliwaumiza wengi akiwemo aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Mwinyi ambaye sasa ni marehemu.

Rais Mwinyi alidiriki kusema Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kwa sababu Simba ilikubali kichapo klcha mabao 2-0 kwenye ardhi ya nyumbani, Simba ilianzia ugenini na ikiilazimisha Stella Abdijan kwenda nayo sare tasa 0-0.

Kipigo Cha mabao 2-0 kiliwaumiza wengi na ikikosa zawadi ya magari aina ya KIA ambapo mfadhili wa zamani wa klabu hiyo Azim Dewji aliahidi kuwapa kila mchezaji endapo Simba itachukua ubingwa.

Simba ikikosa taji hilo mwaka 1993 kabla ya Shirikisho la soka Afrika, CAF kuyaunganisha michuano hiyo na kombe la Washindi na hatimaye kuwa kombe la Shirikisho mwaka 2004 na Simba kufanikiwa tena kuingia fainali mwaka huu 2025.

Kikosi cha Simba msimu huu na kocha wake Fadlu David's raia wa Afrika Kusini wataingia kwenye rekodi za kudumu za klabu hiyo, niwape pongezi sana Simba kwa kuweza kuandikisha historia hiyo ambayo inaweza kudumu kwa vipindi na vipindi.

Naamini mpira wetu umepiga hatua kiasi kwamba vilabu vyetu vinaweza kurudia mafanikio yake kwa msimu na msimu, lakini kitendo cha Simba kufika fainali kinahitaji salamu za pongezi
kutoka kwa kila Mtanzania.

Yanga SC msimu juzi 2023 walikuwa wa kwanza kuandika rekodi ya kuwa timu ya Tanzania kufika fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika na ilicheza na timu ya USM Alger ya Algeria.

Simba nao watacheza na RSB Berkane ya Morocco na ikifanikiwa kuijibu rekodi ya Yanga, ingawa Simba inaweka rekodi nyingine ya kuwa timu ya kwanza nchini kuingia fainali ya pili ya CAF


Wachezaji wa Simba waliopo kwenye cha sasa wanastaili kila aina ya pongezi kwani watakumbukwa katika kipindi chao chote kama kilivyoimbwa kikosi kilichoingia fainali ya kombe la CAF mwaka 1993 ama wa enzi za mwaka 1974 ambapo kilifika nusu fainali ya Klabu Bingwa Afrika.

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...