Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Pyramid Football Club, Klabu changa nchini Misri na maajabu yake

Sio klabu kongwe kwenye soka la Africa na hata kwenye ligi kuu ya Egypt hawana historia kubwa ya mafanikio mwaka huu ndio kwanza wanatimiza miaka 17 baada ya kuanzishwa mwaka 2008.

PYRAMIDS haijawahi kushinda kombe la ligi kuu ya Egypt hata mara moja imeishia tu nafasi ya pili(Runners) ndo mafanikio makubwa kwenye ligi kuu ya Egypt, Kwenye michuano ya CAF mafanikio makubwa ni final ya CAF confederation Cup msimu 2019/20.

Kwenye CAF Champions league ndo wageni kabisa hawajawahi kufika stage kubwa kabisa kwanza hata kushiriki ilikuwa changamoto ila msimu huu wamefanya makubwa sana kuanzia kwenye ligi kuu hadi CAF Champions league ambapo wapo fainali.

KRUNOSLAV JURCìC, kocha mkuu wa Pyramids ameingia kwenye rekodi ya klabu hiyo kwa kuipeleka Pyramid final ya CAF Champions league kwa mara ya kwanza kwenye historia ya klabu hiyo,Sajili za Pyramids za hivi karibuni zilionyesha nini klabu inataka hasa kwenye CAF tournament na sasa kila kitu kipo wazi timu ipo final.

Uwekezaji mkubwa kwenye kikosi cha Pyramids wachezaji kama BLATI TOURE kutoka Burkina Faso amefanya makubwa sana kwenye kikosi uwepo wa FISTON KALALA MAYELE umeongeza nguvu kubwa kwenye safu ya ushambuliaji na uwepo wa nyota wengine kwenye kikosi kumeipa Pyramids nguvu ya kupambana na uwezo wa kushindana kwenye mashindano makubwa.

Lakini pia ongezeko la mchezaji Ramadan Sobhi kwenye kikosi cha Pyramids umeongeza chachu kubwa, Sobhi ni mshambuliaji aliyepata makuzi ya soka pale Al Ahly kabla ya kutimkia Stoke City, Huddersfield na badae kurudi Al Ahly kwa mkopo kisha kujiunga na Pyramids msimu wa 2020.

Alijiunga na Pyramids kwa dau la dola 2M huku akichukua mshahara wa dola 1.4M kwa mwezi, huu ni miongoni kati ya usajili ulioleta chachu na kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Pyramids.

Nb: Kumbe inawezekana klabu kama Pyramids kutunisha msuli mbele ya klabu kubwa kama Al Ahly na Zamalek.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...