KAMPUNI ya vifaa vya michezo na viatu, Diadora ya Italia yenye maskani yake mjini Caerano di San Marco imeingia mkataba wa kuitengenezea jezi klabu ya Simba ya Dar es Salaam.
Akizungumza leo Jijini Durban, Afrika Kusini Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Jayrutty Investment Limited, Joseph Rwegasira amesema kwamba kuanzia msimu ujao Simba itavaa jezi za Diadora.
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu Diadora Afrika Kusini, Yusuf Vadi amesema kwamba ameahidi kutumia fursa hiyo kuendelea kuutangaza ubora wao katika utoaji wa vifaa bora vya michezo.
