Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HONGERA TABIA BATAMWANYA KWA KUSHINDA TUZO

Na Prince Hoza

HONGERA sana tena sana mwanadada Tabia Batamwanya kwa kushinda tuzo ya mwimbaji bora wa muziki wa dansi ilitolewa hivi karibuni, haikuwa rahisi kwa mwanadada huyo kubeba tuzo hiyo kwani ameipigania kwa muda mrefu sana. 

Batamwanya ni msanii wa siku nyingi lakini jina lake limeanza kufahamika hivi karibuni kutokana na kuvuma kwa wimbo wake wa "Narudi nyumbani" aliomshirikisha mwanamuziki wa bongofleva Uncle Some. 

Batamwanya alianza kujulikana tangu mwaka 2006 pale alipojikita kwenye sanaa ya ulimbwende, msanii huyo aliibuka mshindi wa Miss Singida na kufanikiwa kushiriki mashindano ya Miss Tanzania. 

Ikumbukwe Batamwanya alishiriki sambamba na Wema Sepetu ambaye aliibuka mshindi na kuwakilisha Tanzania kwenye Miss World, safari ya Batamwanya kwenye urembo nadhani iliishia hapo na alijikita kwenye muziki wa dansi. 

Batamwanya ni mtoto wa mwanamuziki wa zamani wa muziki wa dansi nchini Jumbe Batamwanya ambaye alihudumu katika bendi ya Bima Lee Orchestra ambapo alijipatia umaarufu mkubwa. 

Historia ya Jumbe Batamwanya aliyetamba na wimbo uitwao "Siri" alipendelea kuambatana steji na mtoto wake wa kike ambaye ndiye huyu Tabia Batamwanya na ilitabiriwa kwamba atakuja kumrithi baba yake miaka ya baadaye atakapokuwa mkubwa. 

Kwasasa Jumbe Batamwanya ametangulia mbele ya haki na Tabia akaamua kumrithi baba yake, kwa bahati mbaya sana Tabia aliangaika bila mafanikio kwani alishiriki kutumikia bendi mbalimbali na kuambulia msoto. 


Mimi binafsi niliwahi kukutana na Tabia ambaye maskani yake ni Manzese Mkunguni jijini Dar es Salaam, alionyesha kutata tamaa kwani muziki wa dansi haukumlipa, Tabia anasema baba yake alipata mafanikio makubwa enzi zake ikiwemo kujenga nyumba ya kuishi na kununua gari. 

Baba yake alifanikiwa kupata ajira katika shirika la Bima na kwakifupi 
alijipatia umaarufu mkubwa, lakini yeye alitaabika na aliona umuhimu wa kuacha muziki wa dansi. 

Kuna wakati alijikita kwenye uigizaji na baadaye akajifunza utangazaji na alihudumu kwenye tv online, binafsi namfahamu vizuri Tabia Batamwanya. 

Lakini sasa amegeuka malkia wa muziki wa dansi hapa nchini, jina la Tabia Batamwanya ndio gumzo kwasasa kwani wimbo wake wa "Narudi nyumbani" imemtambulisha vema, mwanadada huyo akaingia kwenye Top ten za redio mbalimbali hapa nchini. 


Pia staa huyo wa muziki wa dansi akaingia kwenye kuwania tuzo zinazowahusisha wanamuziki wa dansi, nimeamua kumpa hongera kwani tuzo hiyo itamuongezea ari na kasi mpya na kumrejeshea morali ya kuupenda muziki. 

Tayari bendi mbalimbali kubwa hapa nchini zilianza kumuwania ikiwemo Msondo Ngoma, Sikinde Ngoma ya Ukae, lakini Ally Choki kupitia bendi yake ya Extra Bongo wana Next Level imefanikiwa kumchukua na sasa anaitumikia bendi hiyo. 

Tabia Batamwanya anaanza kuhesabu tuzo na akianza na hii ya Cheza Kidansi Awards na baadaye Kilimanjaro Tanzania Music Awards. 

ALAMSIKI  


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe