SIMBA YAWEKA WAZI USHINDI KWAO NI LAZIMA J,PILI

Na Ikram Khamees. Morogoro

Vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, Simba Sc wameahidi kuibuka na ushindi katika mchezo wao dhidi ya mahasimu wao Yanga Sc utakaochezwa Jumapili uwanja wa Taifa  jijini Dar es Salaam.

Watani hao wa jadi wa soka la Tanzania watakutana katika mchezo wa Ligi Kuu bara huku Simba ikiwa kileleni ikifuatiwa na Yanga Sc hivyo kila moja inahitaji ushindi, Timu zote mbili zimejichimbia mjini Morogoro.

Mkuu wa kitengo cha habaro na mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema ushindi kwa klabu yake ni lazima na wala hakuhitaji nguvu kuupata, amedai kikosi chao kimeimarika idara zote hivyo wanazifuata pointi zao Taifa.

Manara ameongeza kuwa msimu huu wanautaka ubingwa wa bara kwa hali yoyote ile na ili ubingwa unoge lazima umfunge Yanga

Simba inaumana na Yanga Jumapili na wamesema watashinda tu hata kwa lazima

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI