Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA NA YANGA LEO NANI ATALALA MAPEMA!

Na Saida Salum. Dar es Salaam

Leo ndio leo asiyekuwa na mwana abebe jiwe ndivyo msemo wa kiswahili unavyoweza kutumika wakati watani wa jadi wa soka la Tanzania, Simba Sc na Yanga Sc watakapoumana jioni ya leo uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Katika kuelekea mchezo huo, Simba wanaonekana wako vizuri kuliko mahasimu wao Yanga ambao mashabiki wake wanaonekana wameikatia tamaa timu yao kutokana na matokeo wanayoyapata kwenye ligi, lakini kwa mujibu wa historia za timu hizo zinapokutana timu inayokuwa imeenea huwa inafungwa na ile inayoonekana dhaifu.

Yanga inaingia uwanjani bila ya kocha wao mkuu, Mzambia George Lwandamina ambaye ameacha kazi na kurejea kwao Zambia na kuna taarifa amejiunga na timu yake ya zamani ya Zesco United, pia inaendelea kuwakosa nyota wake muhimu washambuliaji Donald Ngoma na Amissi Tambwe jambo ambalo linawanyima imani mashabiki wake huku sasa ikipanga kuwategemea Obrey Chirwa, Raphael Daudi, Yusuph Mhilu na Ibrahim Ajibu.

Wakati Simba yenyewe inatambia washambuliaji wake wachana nyavu Shiza Kichuya, Emmanuel Okwi na John Raphael Bocco ambao wameifanya timu hiyo msimu huu kuwa kileleni kwa wingi wa pointi ambazo ni 59 zikiwaacha nyuma sana wapinzani wake kwani Azam Fc wanaoshika nafasi ya pili wana pointi 49 na Yanga inayoshika nafasi ya tatu ina pointi 48.

Yote kwa yote sijui nani atalala mapema leo, timu hizo zote ziliweka kambi mjini Morogoro na kila moja katika mechi zake za ligi Simba ikicheza na Lipuli Fc ilitoka sare ya 1-1 wakati Yanga nao wakacheza na Mbeya City wakatoka sare pia ya 1-1, mgeni rasmi katika mchezo wa leo ni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Poul Makonda

Simba na Yanga zinaumana leo Taifa Dar es Salaam

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe