SIMBA KUSAKA USHINDI MWINGINE KWA LIPULI LEO

Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam

Vinara wa Ligi Kuu Bara Simba Sc jioni ya leo wanakuwa wageni wa Lipuli Fc katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uwanja wa Samora mjini Iringa.

Kwa hakika Simba leo inahitaji ushindi mwingine muhimu ili kujiwekea matumaini ya kutwaa ubingwa msimu huu baada ya kuhangaika kipindi cha miaka mitano bila mafanikio.

Lipuli inayonolewa na kiungo wa zamani wa Wekundu hao wa Msimbazi, Seleman Matola ambaye inaonekana pia ameongezewa nguvu na kocha wa zamani wa Yanga, Kenny Mwaisabula "Mzazi" kwa vyovyote wanataka kuizuia Simba yenye safu kali ya ushambuliaji inayoongozwa na Emmanuel Okwi, John Bocco na Shiza Kichuya

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI