SERENGETI BOYS YABEBA NDOO YA CHALENJI

Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, maarufu Serengeti Boys jioni ya leo imefanikiwa kunyakua ubingwa wa michuano ya Cecafa- Challenge Cup baada ya kuichapa Somalia mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika Burundi.

Ushindi huo wa leo ni dhahiri kwamba itawakilisha vema taifa katika fainali ya mataifa Afrika Afcon- U17 zitakazofanyika mwakani Tanzania ambapo Serengeti itakuwa mwenyeji.

Mabao ya Serengeti Boys yalifungwa na Edson Jeremiah na Jaffari Mtoo, Serengeti ilipenya hatua ya fainali baada ya kuilaza Kenya mabao 2-1 wakati Somalia iliiondosha Uganda kwa kuichapa bao 1-0

Serengeti Boys mabingwa Cecafa Challenge Cup

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI