Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Njombe Mji yajinasua mkiani, Mbeya City nayo yabanwa

Na Mwandishi Wetu. Njombe

Timu ya soka ya Njombe Mji ya mjini Njombe jioni ya leo imeutumia vema uwanja wa nyumbani baada ya kuilaza Ndanda Fc ya Mtwara mabao 2-0 uwanja wa Sabasaba mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Vijana wa Njombe Mji wakicheza mbele ya mashabiki wao wameweza kutakata kwa mabao hayo mawili yaliyowekwa kimiani na Notikeli Masasi na Ahmed Adwale na kuifanya timu hiyo kupanda kwa nafasi moja ikitoka nafasi ya 16 hadi ya 15 huku Majimaji Fc ya Songea sasa ikishikilia mkia, Njombe Mji iliyocheza mechi 25 imefikisha pointi 20.

Nayo Singida United imenusurika kichapo toka kwa Mbeya City baada ya kulazimisha sare na wenyeji wao uwanja wa Sokoine mjini Mbeya jioni ya leo.

Mbeya City walitangulia kupata bao lililofungwa na beki wake Haruna Shamte kabla ya Maliki Antiri kuisawazishia Singida United inayonolewa na Mholanzi, Hans Van der Pluijm

Ligi hiyo inaendelea tena kesho kwa timu ya Majimaji ya Songea na Ruvu Shooting, Mtibwa Sugar dhidi ya Azam Fc na Stand United dhidi ya Kagera Sugar

Njombe Mji Fc leo imeifunga Ndanda Fc 2-0

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe