Mwadui yazidi kuichimbia kaburi Mbao Fc

Na Paskal Beatus. Shinyanga

Timu ya Mwadui Fc ya mjini Shinyanga jioni ya leo imeweza kujinusuru katika janga la kutaka kushuka daraja baada ya kuilaza Mbao Fc ya Mwanza kwa bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara uwanja wa Mwadui Complex.

Ushindi huo unawafanya Mwadui kujiweka pazuri huku kipigo hicho kikizidi kuwachimbia kaburi vijana wa Mbao Fc ambao kwa sasa wako shakani.

Goli pekee lililowapa ushindi Mwadui Fc lilifungwa na Charles Ilanfya kunako dakika ya 29 ambapo liliweza kudumu kwa dakika zote 90 za mchezo

Mwadui Fc imeifunga Mbao Fc 1-0 leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI