Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUELEKEA SIMBA NA YANGA JUMAPILI, REKODI YA KIBADEN YAWAUMIZA VICHWA OKWI, BOCCO NA CHIRWA

Na Paskal Beatus. Dar es Salaam

Mwaka 1977 Simba Sc almaarufu Wekundu wa Msimbazi au wana Lunyasi waliinyanyasa Yanga Sc kwa kuichapa mabao 6-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara uwanja wa Taifa (Sasa Uhuru Stadium).

Mshambuliaji wa Simba wakati huo Abdallah Seif Athuman Kibaden aliifungia Simba mabao matatu katika mchezo huo huku mengine mawili yakifungwa na Jumanne Khamis Masimenti na goli lingine Yanga walijifunga.

Basi mpaka sasa imepita takribani miaka 39 hakuna mchezaji yeyote si wa Simba wala Yanga aliyeweza kumfikia Kibaden kwa kufunga mabao matatu kwenye mchezo mmoja wa watani.

Lakini Jumapili ijayo watani hao wa jadi wa soka la Tanzania wanaumana katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, Simba wao wana washambuliaji watatu ambao wanaweza kufanya lolote katika mchezo huo kwa kuvunja rekodi ya Kibaden.

Simba wanaye Emmanuel Anord Okwi, John Raphael Bocco na Shiza Kichuya ambao wanaweza kumfikia Kibaden ingawa wafanye kazi kwelikweli kuupita ukuta wa Yanga ulio chini ya Kevin Yondan na Abdallah Shaibu "Ninja" au Andrew Vicent "Dante", na Yanga wanao watu hatari kama Obrey Chirwa, Raphael Daudi au Pius Buswita ambao kila mmoja anaweza kuvunja rekodi ya Kibaden.

Ukuta wa Simba una watu mahiri kama Salim Mbonde, Jjuko Murushid au Yusuph Mlipili ambapo unaweza usiamini kuwa huenda Kibaden akaendelea kutesa na rekodi yake ya Hat trick ndani ya Simba na Yanga "Derby"

Abdallah Kibaden (Pichani) rekodi yake huenda ikavunjwa Jumapili

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe