Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Taarifa za Mkude kuvunjika kifundo cha mguu hizi hapa

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Kiungo mahiri na bora kwa sasa hapa nchini, Jonas Gerald Mkude jana amevunjika kifundo cha mguu akiwa katika mazoezi ya klabu yake ya Simba Sc  yaliyofanyika kwenye uwanja wa Boko Veteran.

Taarifa ambazo Mambo Uwanjani imezinyaka, zinasema kuwa kiungo huyo aliumia kifundo cha mguu na kushindwa kuendelea na mazoezi na kupelekea kurudishwa nyumbani kwake ni baada ya kufanyiwa rafu na kiungo mwenzake Muzamir Yassin.

Daktari wa Simba, Yassin Gembe alishindwa kumpa matibabu kiungo huyo ili arejee mazoezi na badala yake alimruhusu aondoke huku akishindwa kukanyaga kwa miguu yote miwili kwani alikuwa akichechemea, Simba inajiandaa na mchezo wake wa Ligi Kuu bara dhidi ya Njombe Mji, Aprili 3 mwaka huu uwanja wa Sabasaba mjini Njombe hivyo kunatilia shaka uwepo wa Mkude katika mchezo huo.

Licha ya kuumia Mkude, jana majeruhi wawili wa muda mrefu, Haruna Niyonzima na Salim Mbonde wameanza mazoezi na kuna uwezekano mkubwa wa kuanza katika mchezo huo, Simba ndio kinara wa ligi hiyo ikiwa na pointi 46 lakini ikilingana na hasimu wake Yanga Sc

Jonas Mkude ameumia

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe