Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ANAYEKUMBUKWA

ISSA ATHUMAN MGAYA: FUNDI WA MPIRA.

Alianza kujulikana kama fundi seremala akitengeneza vitanda, makochi na meza kwa kutumia mbao, ujuzi huo alifundishwa na mjomba wake ambaye alizaliwa tumbo moja na mama yake mzazi.

Hapa namzungumzia fundi wa mpira Issa Athuman Mgaya ambaye alicheza kwa mafanikio Yanga Sc na timu ya taifa, Taifa Stars miaka iliyopita.

Nakumbuka wakati huo nilikuwa mdogo lakini nilikuwa mfutiliaji mkubwa wa mpira wa miguu, Issa alikuwa kiungo mkabaji wa Yanga mwenye uwezo wa kucheza sentahafu na aliweza kung' ara vilivyo kwenye kikosi hicho na kubahatika kwenda kucheza soka la kulipwa Uarabuni.

Kwa miaka hiyo mchezaji wa Kitanzania ukisikia anaenda Uarabuni ujue huyo ni staa kwelikweli, basi Issa alibahatika kwenda Umangani, na aliporejea nchini alijiunga tena na Yanga.

Nakumbuka kipindi hicho Yanga ilikuwa na nyota kama Steven Nemes, Seleman Mkati, Kenneth Mkapa, Godwin Aswile, Salum Kabunda, Abubakar Salum "Sure Boy" Justin Mtekele, Said Mwamba, Edibili Lunyamila, Mohamed Hussein "Mmachinga" na wengineo.

Kitu cha kukumbuka kwa Issa Athuman ambaye mdogo wake ni Kassongo Athuman alikuwa anaichezea Simba, siku moja Simba na Yanga ziliumana uwanja wa Taifa wakati ule na sasa ni Uhuru, wachezaji hao wawili kila mmoja alichezea timu yake.

Basi bwana beki wa Yanga enzi hizo Salum Kabunda "Ninja" aliyesifika vibaya kwa kucheza rafu, alimrukia kifuani na miguu yote miwili beki wa Simba Kassongo Athuman ambaye alikuwa na desturi ya kupandisha mbele mashambulizi.

Ninja alitaka kumuua kabisa Kassongo kwani ilibidi awahishwe Muhimbili kufuatia rafu mbaya aliyochezewa na Ninja ambaye kwa sasa naye ni marehemu, baada ya Kassongo kuumizwa vibaya, Issa Athuman siku ile alikuwa nahodha wa Yanga alikasirishwa na rafu ya Ninja na kumfuata kwa karibu akitaka kumchapa.

Hapo ndipo ikaibuka songombingo kati ya Issa wa Yanga na Ninja pia wa Yanga, kweli damu nzito kuliko maji, Issa ameipa Yanga mataji kadhaa likiwemo kombe la Kagame

Kikosi cha Yanga kilichotwaa klabu bingwa Afrika mashariki na kati, Kampala, Uganda

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe