Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA YATHIBITISHA KUSHIRIKI KAGAME

Uongozi wa klabu ya Yanga umekanusha taarifa kwamba umejitoa katika Kombe la Kagame la klabu bingwa ya Afrika Mashariki na Kati nchini Rwanda kama ambavyo imeripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini.

Yanga imesema itashiriki michuano hiyo ya kila mwaka, baadaye mwezi ujao, endapo itaarifiwa rasmi na Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ambao ndiyo waandaaji.


Akizungumza jana, Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema uongozi haujatangaza kokote kwamba Yanga haitakwenda Rwanda, isipokuwa imekuwa ikisema haina taarifa zozote juu ya ushiriki.

Kizuguto alisema Yanga haina sababu ya kutoshiriki michuano hiyo, lakini ni vigumu kusema lolote wakati haina taarifa zozote kutoka CECAFA.

"Bado hatujapata taarifa zozote na hatujatoa msimamo juu ya ushiriki wetu, hizo taarifa kwamba sisi hatuendi zinatoka wapi?" aliuliza Kizuguto.
"Subiri CECAFA watuletee taarifa za kimaandishi muone kama Yanga itakwenda Kagame au haiendi.

"Yanga haina haja ya kuwa na hofu juu ya michuano hiyo kwa sababu ina kikosi imara na kocha bora (Marcio Maximo)."

Makocha wa Yanga: kikosi kipo tayari kwa kushiriki kagame

Hata hivyo kauli ya Kizuguto inatofautiana na taarifa za Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka (TFF) kuwa, Selestine Mwesigwa kwamba Yanga inazo taarifa juu ya michuano hiyo kwa sababu amekuwa akiwasiliana nayo.

"TFF ni TFF na Yanga ni Yanga. Ukweli ni kwamba hatuwezi kuwa watoto wadogo kuongopa hakuna taarifa wakati tunazo," alisema Kizuguto na kueleza zaidi, "uongozi haujafahamishwa na ndivyo hali ilivyo.

"Ila kuhusu ushiriki au kutoshiriki hatujaamua kwa vile hatuna taarifa rasmi sasa tutaamuaje?"

Yanga iliyotwaa ubingwa wa Kagame mara mbili mfululizo mwaka 2011 na 2012 kati ya jumla ya mataji matano iliyonayo, ilishindwa kwenda kujitetea mwaka jana michuano ilipofanyikia Sudan Kaskazini kwa hofu ya usalama.



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe