Ruka hadi kwenye maudhui makuu

USAJILI ULAYA WAZIDI KUPAMBA MOTO

Manchester United wamerejea tena kumfuatilia winga wa Real Madrid Angel Di Maria, 26, baada ya jaribio la kwenda Paris Saint Germain kugonga mwamba kuhusiana na ada ya uhamisho ya pauni milioni 45 (Sun)

Southampton wanataka kubaki na kiungo wao Morgan Schneiderlin, 24, na watawaambia Tottenham na Arsenal watahitaji kutoa zaidi ya pauni milioni 27 kama wanamtaka (Guardian)

Boss mpya wa Southampton, Ronald Koeman amekataa pauni milioni 3.25 kutoka Cardiff kumsajili beki Jose Fonte, 30 (Daily Mirror)


Barcelona wanafikiria kumchukua beki wa kati Thomas Vermaelen, 28, kutoka Arsenal, ambaye pia anasakwa na Manchester United (Sun), Arsenal wamepewa nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli, 23, kwa pauni milioni 7.9 pamoja na kubadilishana na winga kutoka Costa Rica, Joel Campbell (Metro)

QPR wanazungumza na Marseille kumchukua kiungo wa Ufaransa Mathieu Valbuena, 29, ingawa Dynamo Moscow pia wanamtaka (Daily Mirror), Everton wana matumaini ya kukamilisha uhamisho wa pauni milioni 18 wa mshambuliaji wa Chelsea, Romelu Lukaku, 21 baada ya kuwasili kwa Didier Drogba, 36, Darajani (Daily Express)

Everton pia wanatazama uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Monaco Lacina Traore, 23, kwa mkopo (Times), boss wa Roma Rudi Garcia amesema kiungo Kevin Strootman, 24, hana mpango wa kwenda Mancheter United msimu huu (Sky Sports)

Liverpool wametoa dau la pauni milioni 14.2 kumtaka winga wa Bayern Munich Xherdan Shaqiri, 22 (Daily Star), West Ham wamekuwa na mazungumzo na mshambuliaji wa Besitkas Hugo Almeida, 30, baada ya Andy Carroll kuumia (Times)

Atlètico Madrid wanamtaka mshambuliaji wa Real Sociedad, Antoinne Griezmann, ambaye anafuatiliwa na Tottenham pia (Daily Express), mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney, 28, anataka kuwa nahodha wa klabu hiyo na anaamini huenda akalibeba Kombe msimu unaokuja (Manchester Evening Standard)

Kiungo wa Man U Tom Cleverly, 24, ana uhakika atarejea katika 'form' chini ya Louis van Gaal baada ya kuwa na wakati mgumu enzi za David Moyes (ESPN), Wojciech Szcesny, 24, atasalia kuwa kipa namba moja wa Arsenal licha wa kuwasili kwa David Ospina, 25 kutoka Nice (Daily Express)

Chelsea bado wanamfuatilia beki wa Real Madrid Rafael Varane, ambaye yupo katika mazungumzo juu ya mkataba mpya (The Independent), Real Madrid huenda wakamchukua mshambuliaji wa Colombia Radamel Falcao kwa mkopo na mshahara wa euro milioni 12 kwa mwaka (ABC)

Everton wanamfuatilia kwa makini winga wa AIK Nabil Bahoui, 23 (Sky Sports), Edinson Cavani anataka kuondoka Paris Saint-Germain, huku Manchester United wakiwa wanamtazama mchezaji huyo wa Uruguay (Le 10 Sport)

Hatma ya Angel Di Maria inatarajiwa kuamuliwa siku chache zijazo, huku Real Madrid wakiwa tayari kupokea dau la euro milioni 50 hadi 60 kutoka kokote (Cadena Cope)

Liverpool huenda wakamkosa Divock Origi baada ya Atlètico Madrid kumtaka mchezaji huyo wa Ubelgiji, kufuatia kuondoka kwa Diego Costa, Adrian na David Villa (Marca) Arsenal wanakaribia kumsajili beki Calum Chambers kutoka Southampton (Sky Sports)

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe