Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UJERUMANI MBABE ZAIDI YA ARGENTINA HISTORIA HIYO

Mara ya mwisho Argentina kukutana na Ujerumani katika Fainali 1986.
Argentina na Ujerumani zitachuana kwa mara ya 3 katika fainali ya kombe la dunia.
Je wajua itakuwa mara ya 8 kwa timu hizo kuchuana katika kombe la dunia ?
Ukinzani wa jadi kati ya Brazil-Argentina unaweza kumithilishwa tu na uhasama baina ya Ujerumani na Uholanzi.


Lakini baada ya Argentina kutinga fainali ya kombe la dunia huko Brazil dhidi ya Ujerumani Uhasama wa kikanda baina ya Argentina na Brazil umeibuka upya.

Mashabiki wa Brazil wanaona kheri kushabiki Ujerumani iliyowaadhibu mabao 7-1 kuliko kuitizama timu wanayoichukia zaidi Argentina ikitazwa mabingwa wa kombe la dunia mwaka wa 2014 nchini Brazil,,ni kama msumari kwenye kidonda anasema Sanche raiya wa Brazil.

Maoni yake yanafanana na maelfu kama si mamilioni ya wa Brazil .
Argentina itakuwa inakutana na Ujerumani kwa mara ya tatu katika fainali ya kombe la dunia ambayo ni rekodi mpya baina ya mahasimu hao wawili.
Mfungaji mabao mengi ya kombe la dunia Klose
Aidha Argentina imekutana na Ujerumani katika mechi zingine 5.
1958
Wajerumani wakiwa ndio mabingwa watetezi wa kombe la dunia Ujerumani waliibuka washindi mabao win 3-1.
1966
Ujerumani ilitoka sare tasa na Argentina katika mechi za mkondo wa kwanza .
1986 Fainali
Argentina iliibuka washindi kwa mabao 3-2 .
Huu ndio mwaka ambao Mshambulizi wa Argentina Diego Maradona alifunga kwa mkono timu hizo zilipokuwa zimetoshana nguvu 2-2 hadi katika dakika ya 84 ya kipindi cha pili.

1990 Fainali
UJerumani iliibuka washindi kwa bao moja kwa nunge kupitia penalti ya dakika ya 85 katika kipindi cha pili.
2006 (Robo fainali)
Messi kuiongoza Argentina dhidi ya Ujerumani
Huu ndio mwaka ambao Wajerumani walikuwa wenyeji wa kombe la dunia.
Argentina walikuwa wamewadhibiti wenyeji wao huko Berlin mechi hiyo ilipokamilika 1-1 katika muda wa ziada .

Die Mannschaft walijifurukuta na kuilaza Argentina 4-2 kupitia mikwaju ya penalti.(Ujerumani hatimaye ilishindwa na Italia katika nusu fainali)
2010 (Robo fainali)

Hii ndilo lililokuwa kombe la dunia la kwanza kuandaliwa katika bara la Afrika na mahasimu hao walikutana katika hatua ya robo fainali Argentina ikifunzwa na nyota wao Maradona.
Thomas Müller aliiongoza Ujerumani kuititima Argentina mabao 4-0 .
Mechi hii ndiyo iliyodhibitisha Thomas Müller na Miroslav Kose ni wa shambulizi wenye haiba ya juu.
Kuanzia wakati huo Argentina wamekipika kikosi chao upya sasa wakimtumia nyota wao Messi kama mshambulizi wa pekee.

Hiyo yote ni Historia je Jumapili ni nani atakayeibuka mshindi ?
Ujerumani ambayo kila mchezaji anauwezo wa kufunga mabao ama Argentina yenye uwezo mkubwa lakini ikimtegemea Messi kuifikisha kwenye Fainali ?

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe