Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STRAIKA WA IVORY COAST AMALIZANA NA SIMBA

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Taifa ya Burundi, Pierre Kwizera, ambaye alikuwa nchini akifanya mazungumzo na uongozi wa Simba, ameondoka juzi usiku kurejea Ivory Coast kwa lengo moja la kwenda kuvunja mkataba na klabu yake ya Afad Abdijan.

Mchezaji huyo anayecheza nafasi zaidi ya mbili uwanjani, amewaambia viongozi wa Simba kwamba atahakikisha anamalizana na Afad Abdijan na kurejea jijini Dar es Salaam kuitumikia klabu hiyo katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

"Kuna mambo naenda kumalizia huko, ila nitarudi Tanzania kucheza Simba," alisema kwa kifupi mchezaji huyo.

Habari kutoka uongozi wa Simba zinaeleza kuwa mchezaji huyo atarejea jijini Agosti 28, mwaka huu tayari kuanza mazoezi na wachezaji wenzake wa timu hiyo.


Kiongozi huyo alisema kuwa Kwizera, amepanga kumalizana kwa busara na viongozi wake wa klabu hiyo ya Ivory Coast ndipo asaini mkataba mpya na Simba.

"Ila ametuhakikishia anarejea Simba," alisema kiongozi huyo ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Kamati ya Usajili.
Simba inajipanga kuimarisha kikosi ili iweze kurejesha heshima yake iliyopoteza msimu uliopita kwa kumaliza ikiwa katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi.

Pia, Simba bado iko katika mipango ya kumnasa kiungo mshambuliaji wa timu ya KCB na timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars), Paul Kiongera.

Rais wa Simba, Evans Aveva, yupo Nairobi, Kenya kukamilisha mazungumzo na nyota huyo ambaye alishawahi kufanya kazi na Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, katika timu ya Gor Mahia.

Azam ndio mabingwa wa msimu uliopita huku Yanga ikiwa ya pili na timu iliyoshiriki kwa mara ya kwanza, Mbeya City, ilimaliza ligi ikiwa ya tatu.

Kikosi cha Simba cha msimu ujao kitatambulishwa rasmi katika Tamasha la Simba Day ambalo mwaka huu litafanyika Agosti 9 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe