Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIRI YA KUTEMWA BIN KLEB YANGA HII HAPA....

WAKATI kukiwa kuna sintofahamu juu ya Mwenyekiti wa klabu ya Yanga SC, Yussuf Manji kuunda Kamati mpya ya Utendaji ya klabu hiyo akiwaweka nje Wajumbe kadhaa, akiwemo Abdallah Bin Kleb, imefahamika kiongozi huyo aliomba mwenyewe kujitoa.

Ingawa sababu haswa ya Bin Kleb kujitoa haijulikani, lakini chanzo cha karibu na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, kimesema kwamba sababu za kupata muda wa kutosha kwa ajili ya biashara zake.

“Abdallah kwa muda mrefu alikuwa anaomba udhuru ili kushughulikia biashara zake ambazo zilikuwa zinakosa usimamizi wa uhakika kutokana na muda wake mwingi kufanya kazi za Yanga,”.


“Shughuli za Dar es Salaam alikuwa anazisimamia vizuri, lakini zile za nchi jirani zilikuwa zinakosa usimamizi kwa sababu muda mwingi yupo na Yanga, kabla ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu (msimu uliopita) aliomba udhuru,”.

“Na baada ya mzunguko wa kwanza pia aliomba udhuru, yote kwa sababu ya kwenda kusimamia biashara zake, sasa baada ya kuona kabisa bila kujitoa moja kwa moja, biashara zake zitayumba akamuomba Manji mapema, akiteua Kamati mpya, yeye asimuweke,”kimesema chanzo hicho.

“Manji alimkatalia mara ya kwanza, lakini ikafika wakati ikabidi amkubalie kwa sababu yeye mwenyewe Abdallah ameahidi kuendelea kuusaidia uongozi kila atakapokuwa anapata nafasi,”kimeongeza chanzo hicho.

Bin Kleb aliingia kwa pamoja na Manji, Makamu Clement Sanga na Wajumbe George Manyama na Aaron Nyanda katika uchaguzi mdogo mwaka juzi, akiwa mgombea aliyepata kura nyingi zaidi ya wengine wote.

Na katika kipindi chake, aliiwezesha Yanga kusajili wachezaji wa kiwango cha juu kama Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Frank Domayo, Didier Kavumbangu, Emmanuel Okwi, Juma Kaseja na wengineo.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano pia, chini yake Yanga SC ilitwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame na Ligi Kuu pamoja na kuweka rekodi ya kuifunga kwa mara ya kwanza timu ya Misri, kwenye michuano ya Afrika, Al Ahly 1-0 mwaka huu.
 
Bin Kleb akiwa ameshika kwa pamoja Kombe la Kagame na Sanga
Seif Magari kushoto akimpongeza Bin Kleb kwa kufanikisha kumrejesha Mrisho Ngassa Yanga. Kulia kabisa ni Mussa Katabaro
Wanachama wengi wa Yanga SC bado wanaamini Bin Kleb kwa kushirikiana na ‘sahiba’ wake Ahmed Seif ‘Magari’ ndio wanaweza kupambana na Friends Of Simba ambao kwa sasa wameshika hatamu Simba SC.

Wana Yanga pia bado wanaamini kukosekana kwa Bin Kleb itakuwa pigo kwenye klabu hiyo, hususan katika sekta ya ‘fitna’ dhidi ya wapinzani wao kwenye utawala wa soka ya Tanzania kwa ujumla, Simba SC.
 
Jana, Mwenyekiti wa Yanga SC, Yussuf Manji alitangaza Kamati mpya ya Utendaji ya klabu hiyo, ambayo pamoja naye kama Mwenyekiti na Sanga Makamu wake, Wajumbe ni Abubakar Rajabu atakayesimamia pia Mradi wa Jangwani City, Sam Mapande atakayesimamia pia Sheria na Utawala Bora, George Fumbuka atakayesimamia pia Uundwaji wa Shirika, Waziri Barnabas atakayesimamia pia Vibali vya Hatimiliki na Mahusiano na Wafadhili, Abbas Tarimba atakayesimamia pia Mipango na Uratibu, Isaac Chanji na Seif Ahmed ‘Magari’ watakaosimamia pia Uendelezaji wa Mchezo, Mussa Katabalo atakayesimamia pia Mauzo ya Bidhaa, Mohammed Bhinda atakayesimamia pia Ustawishaji wa Matawi, David Ndeketela Sekione atakayesimamia pia Uongezaji wa Wanachama, Mohammed Nyenge atakayesimamia pia Utangazaji wa Habari, Taarifa na Matangazo.

Wajumbe hao, pia wataongoza Kamati ndogo ndogo, Mapande za Kamati ya Maadili, Nidhamu na Uchaguzi, Fumbuka na Barnabas Kamati ya Uchumi na Fedha Chanji na Magari Kamati za Ufundi, Mashindano naSoka la Vijana na Wanawake.

Wajumbe waliotemwa mbali na Bin Kleb ni Salum Rupia, Manyama, Nyanda na Lameck Nyambaya.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe