Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTUNISI ADAIWA KUMVISHA PETE YA UCHUMBA VJ PENNY, MWENYEWE AKANUSHA

Latest buzz is about Mtunisy kumvisha pete ya uchumba VJ Penny hivi juzi kati. Kwa mujibu wa chanzo kimoja kilicho karibu na Penny kikizungumza na burudani. kilisema kuwa Mtunisy amemvisha Penny pete hiyo kwa siri kubwa na wamekuwa karibu kwa muda sasa bila hata watu wao wa karibu kujua.

Habari zaidi zinadai kuwa Penny yupo tayari kuolewa na Mtunisy kama mke wa pili ndiyo maana kwa muda sasa amekuwa akivaa ushungi licha ya kuwa mkristu ili akubalike ukweni ambapo Mtunisy ni muislamu.

"Mtunisy kamvisha VJ Penny pete ya uchumba mna taarifa? ilitokea hivi juzi walifanya siri sana hata mimi nilijua baadaye, wapo karibu siku hizi hata Penny anavaa ushungi ili akubalike kwa wakwe zake, Penny amechoka na upweke tangu aachane na Diamond"


Baada ya kupata habari hizo juzi ilibidi kumsaka VJ Penny ili atolee ufafanuzi hata hivyo juhudi ziligonga mwamba lakini Mtunisy alipatikana na alipoulizwa kuhusu kumvisha pete ya uchumba VJ Penny aling'aka na kusema hata hana namba ya Penny walikutana kikazi wakati wa kushuti kipindi kipya cha TV cha

VJ Penny "Dah huo ni uzushi tu hakuna kitu Kama hicho hata namba ya huyo mtu sinayo nilikuwa Nae kwenye kipindi cha Bongowwod tu"Siku chache zilizopita VJ Penny aliweka picha Instagram akiwa amevaa pete ya uchumba lakini hakutaja mwanaume ambaye amemvisha pete hiyo kiasi cha wafuatilia habari za mastaa kuanza kumfuatilia Penny kujua anatoka na nani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe