Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAXIMO AMREJESHA NSAJIGWA YANGA

KOCHA mpya wa Yanga SC, Mbrazil Marcio Maximo amemrejesha beki wa zamani wa timu hiyo, Nsajigwa Joel Shadrack Mwandemele ‘Fusso’ katika timu hiyo.

Maximo alifanya kazi na Nsajigwa katika miaka yake minne ya kuifundisha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na alimpa Unahodha katika miaka yake miwili ya mwisho.

Hiyo ilifuatia kustaafu kwa Manahodha wake wawili wa awali, kwanza Mecky Mexime na baadaye Salum Swedi ‘Kussi’ na Nsajigwa aliendelea kuwa Nahodha wa Stars mbele ya kocha aliyemfuatia Maximo, Jan poulsen kabla ya kustaafu mwaka jana.


Na baada ya kurudi Tanzania kama kocha wa Yanga SC, Maximo amemkumbuka askari wake huyo wa zamani na kumrejesha Jangwani, ingawa safari hii harejei kama mchezaji, bali kocha.

Maximo amemrejesha Nsajigwa Yanga ili awe kocha wa kikosi cha vijana wa timu hiyo, maarufu kama Yanga B, wakati aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Salvatory Edward Augustino ‘Doctor’ anaingia kwenye benchi la ufundi la kikosi cha kwanza.

Maximo amevutiwa na utendaji wa kiungo wa zamani wa Yanga SC, Salva na ameona bora awe naye moja kwa moja kama Msaidizi wake wa kikosi cha kwanza na timu ya pili, iende kwa Nsajigwa.

Juma Pondamali ‘Mensah’ anaendelea kuwa kocha wa makipa, wakati Mbrazil mwingine, Leonardo Neiva anaendelea kuwa kocha Msaidizi Mkuu.

Yanga SC kwa sasa ipo kweye mazoezi makali, ikijiandaa na michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, inayotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao mjini Kigali, Rwanda.

Yanga SC inatarajiwa kuingia kambini Bagamoyo wakati wowote kwa maandalizi zaidi ya michuano hiyo, ambayo wamepangwa kundi A pamoja na wenyeji, Rayon Sport, KMKM ya Zanzibar, Coffee ya Ethiopia na Atlabara ya Sudan Kusini.

Kundi B lina timu za APR ya Rwanda, KCC ya Uganda, Flambeau de L’Est ya Burundi, Gor Mahia ya Kenya na Telecom ya Djibouti, wakati Kundi C linaongozwa na mabingwa watetezi, Vital’O ya Burundi, El Merreikh ya Sudan, Polisi ya Rwanda na Benadir ya Somalia.

Timu 14 zinatarajiwa kushiriki michuano hiyo kuanzia Agosti 8 hadi 24 mwaka huu- jumla ya mechi 34 zikichezwa katika viwanja vya Amahoro na Nyamirambo, Kigali.

Nsajigwa alikuwa Nahodha wa Stars wakati wa Maximo, hapa anakabiliana na Robinho katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Brazil

Rais Paul Kagame wa Rwanda ndiye mlezi wa mashindano haya ambaye hutoa dola za Kimarekani 60,000 kila mwaka kwa ajili ya zawadi.

Wizara ya Michezo ya Rwanda na mashirika mengine yatadhamini michuano hiyo, itakayokwenda sambamba na maazimisho ya miaka 20 ya mauwaji ya kimbau.

Televisheni ya kulipia ya Supersport ya Afrika Kusini ambao ni maswahiba wa muda mrefu wa CECAFA, ni miongoni mwa wadhamini pia na wataonyesha mechi zote za michuano hiyo moja kwa moja. Ratiba ya mashindano hayo inatarajiwa kutolewa wiki hii.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe