Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LIVERPOOL YAMSAJILI MARKOVIC KWA PAUNI MIL 20

Liverpool imetumia £20m kumsajili Markovic
Pauni millioni 20 ndicho kima imekitumia Liverpool kumhamisha Lazar Markovic kutoka Benfica.
Mserbia huyo aliiwezesha Benfica kutwaa taji la Ureno msimu uliopita na anasema anamatumaini makubwa ya kuwaridhisha mashabiki na mwenye club hiyo.

Maneno hayo ya busara yanahitajika sana huko Liverpool baada ya nyota wao Suarez kufifizwa na kashfa ya kung'ata wachezaji wenzake hasa katika mhadhara wa jukwaa la kombe la dunia.
Hata hivyo hilo halijashukisha dau la Suarez sanaa kwani Liverpool waatavuna £75m kutoka Barcelona ambako Suarez sasa amepata makao mapya.

Hivyo ili kujiimarisha kwa kampeni yao ya msimu unaokuja wa Champions League na Premier League walioambulia nafasi ya pili kinyume na matarajio ya wengi, Markovich mwenye umri wa miaka 20 anakuwa mchezaji wa nne kupata mkataba na Liverpool hivi karibuni.
Je Liverpool itatumia pesa ngapi kumsajili mshambuliaji chipukizi Origi
Wengineo ni Mshambuliaji Rickie Lambert, 32 kwa pauni £4m na Adam Lallana, mwenye umri wa miaka 26, kwa pauni £25m, wote walitokea Southampton.

Kumbuka Liverpool pia inasubiri uamuzi wa Divock Origi, mwenye asili ya Kenya , aliyatamba kweli katika safu ya ushambuliaji akiwa kombe la dunia na timu yake ya Ubeleji.

Kweye umri wa miaka 19 pekee wengi wanasubiri kwa hamu kuona Je Liverpool itatumia pesa ngapi kumpata Origi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe