Ruka hadi kwenye maudhui makuu

IVO MAPUNDA AMUHOFIA CASSILAS


Kipa chaguo la kwanza wa timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Ivo Mapunda, amesema kwamba anamhofia kipa mpya aliyetua kwenye kikosi hicho, Hussein Shariff 'Casillas' kutoka Mtibwa Sugar ya Manungu mkoani Morogoro.

Casillas alisaini mkataba mpya wa miaka miwili wa kuitumikia Simba mwishoni mwa wiki iliyopita.

Akizungumza na gazeti hili, Mapunda, alisema kwamba Casillas ndiye kipa bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita hivyo atajipanga kufanya mazoezi ili kulinda kiwango chake na kujihakikishia namba katika kikosi cha kwanza.


Mapunda ambaye aliwahi kuzichezea timu za Prisons ya Mbeya, Yanga ya jijini na St. George ya Ethiopia alisema kuwa hatabweteka na atahakikisha anapambana ili kulinda nafasi yake kama ilivyokuwa msimu uliopita.

Cassilas ameanza kumtisha Mapunda baada ya kutua Simba akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro

Aliongeza kuwa kila mchezaji kwenye timu hana uhakika wa namba ndiyo maana wanapokuwa mazoezini wanajituma na kumshawishi kocha kuwapa nafasi.

"Casillas ni kipa bora msimu uliopita, hivyo ni mzuri na mimi nimejipanga kukabiliana na changamoto hiyo, pia naamini kila mmoja atahakikisha anamridhisha mwalimu," alisema kipa huyo.

Simba tayari imeshaanza kujifua kujiandaa na msimu mpya wa Ligi ya Bara na jana jioni Mcroatia, Zdravko Logarusic, alikiongoza kikosi chake kwa mara ya kwanza tangu arejee kutoka likizo kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu Mlimani.

Hata hivyo Simba kama zilivyo timu nyingine zenye wachezaji katika timu ya Taifa (Taifa Stars) itawakosa nyota wake wa kikosi cha kwanza katika maandalizi.

Nyota hao ni pamoja na Amri Kiemba, Haroun Chanongo, Jonas Mkude, Ramadhani Singano 'Messi' na Joram Mgeveke walio katika kambi ya timu ya Taifa Stars wakati Amissi ambwe naye ameitwa kwenye timu ya taifa ya Burundi huku baadhi wakiwa bado hawajaripoti mazoezini akiwamo beki, Donald Musoti.

Simba ilimaliza msimu uliopita ikiwa katika nafasi ya nne na hivyo mwakani haitashiriki mashindano yoyote ya kimataifa wakati mabingwa ni Azam ambao watashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Kagame huku Yanga walioshika nafasi ya pili watapeperusha bendera ya Bara kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe