Ruka hadi kwenye maudhui makuu

GOTZE ASEMA, LILE LILIKUWA BAO LA NGEKEWA TU KWAKE.

Shujaa wa Ujerumani, Mario Gotze amesema kufunga bao pekee na la ushindi katika fainali ya Kombe la Dunia ni kama bahati na zawadi yake katika msimu wake mgumu akiwa Bayern Munich.

Gotze (22), mwenye sura ya kitoto, alituliza kifuani mpira wa krosi ya Andre Schuerrle kabla ya kupiga shuti kufunga bao katika dakika ya 113, na kuipa Ujerumani ushindi 1-0 dhidi ya Argentina kwenye Uwanja wa Maracana, Rio de Janeiro, Brazil.


“Ni hisia ambazo siwezi kuziamini wala kuzielezea,” alisema kiungo huyo wa Bayern.

“Sijui hata nilielezee vipi hili. Unajikuta unafunga bao na hujui kitu kitakachotokea. Itakuwa ni sherehe pamoja na timu nzima na taifa kwa ujumla.  Ni kama ndoto iliyotimia.”

Gotze aliingia kuchukua nafasi ya mkongwe Miroslav Klose kabla ya kuanza kwa muda wa nyongeza. Hilo ni bao lake la 11 kuifungia timu ya taifa katika michezo 35 aliyoitumikia miamba hiyo maarufu kama ‘Die Mannschaft’.

Alitwaa pia tuzo ya mchezaji bora wa mechi, ambayo alipewa uwanjani hapo wakati Ujerumani ikiweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kutoka Bara la Ulaya kutwaa taji hilo katika ardhi ya bara la Amerika Kusini.

Gotze anaungana na ‘Der Bomber’ Gerd Mueller, ambaye alifunga bao la ushindi kwa Ujerumani Magharibi katika mchezo wa fainali 1974 mjini Munich, akiwa mchezaji mwingine wa Bayern kulipa ubingwa taifa hilo.

Gotze alitua nchini Brazil akiwa ametokea kwenye hali ngumu katika msimu wake wa kwanza na miamba hiyo ya Bavaria, akiwa ameshindwa kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha kocha Pep Guardiola.

Akiwa ametwaa mataji mawili ya Bundesliga na Borussia Dortmund, klabu ambayo alijiunga nayo akiwa na miaka nane, Gotze alikuwa adui namba moja wa mashabiki wa Borussia Aprili 2013, alipokubali uhamisho wa Euro 37 milioni ili kujiunga na Bayern.

Uhamisho huo umemfanya nyota huyo kuipa kisogo timu iliyomkuza na ya nyumbani kwao. Alikuwa nje katika mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Mei 2013, baada ya kuumia katika mchezo wa nusu fainali ya michuano hiyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe