DJOKOVIC AMZIMA FEDERAR WIMBLEDON

Djokovic ndiye bingwa wa Wimbledon
Mchezaji tenis wa Serbia Novak Djokovic ndiye bingwa wa mwaka huu wa kombe la Wimbledon.
Djokovic alimlaza Mswisi Rodger Federer seti tatu kwa mbili za alama 6-7 (7/9), 6-4, 7-6 (7/4), 5-7, 6-4 katika fainali hizo za wanaume..

Bingwa huyo wa mwaka wa 2011 alitamatisha msururu wa kushindwa kwa mataji makuu ya Grand Slam alipoandikisha taji lake kuu la 7 .
Mchezji huyo mwenye umri wa miaka 27 alishangilia ushindi huo wa kihistoria kwa kupigasijida katikati ya uwanja wa kati huko wimbledon na kutafuna nyasi asijue aliwahi vipi kumkomesha federer ambaye alikuwa anatafuta taji lake la nane na la kuvuweka rekodi mpya.
Iwapo angeshinda Federer angekuwa ndiye mchezaji mkongwe zaidi kuwahi kutaa ubingwa huo akiwa na umri wa miaka 32 .
Rekodi ya sasa inashikiliwa na Pete Sampras ambaye ameshinda mataji saba sawa na Federer.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI