Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RWANDA YAMTAKA STEPHEN CONSTANTINE

Constantine anatazamiwa kufanya mazungumzo na shirikisho hilo la Ferwafa Alhamisi.
Timu taifa ya soka ya Rwanda inamtaka Raia Muingereza Stephen Constantine kuwa mkufunzi wake katika mkataba wa miaka miwili.


Tayari shirikisho la soka nchini humo limempendekezea mkataba wa miaka miwili.
Shirikisho la kandanda la taifa hilo linamtaka mkufunzi atakayechukua usukani baada ya Eric Nshiyamana, ambaye mkataba wake na timu hiyo utatamatika tarehe 31 mwezi Julai.

Kocha huyo wa zamani wa Millwall mwenye umri wa miaka 51, ana uzoefu wa kandanda ya bara la Afrika, hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa mkufunzi wa timu ya taifa ya Malawi tangia mwezi Februari mwaka wa 2007 hadi Aprili mwaka wa 2008.

Constantine anatazamiwa kufanya mazungumzo na shirikisho hilo la Ferwafa Alhamisi.
Msemaji wa Shirikisho la Soka la Rwanda bwana Vedaste Kayiranga aliiambia BBC kwamba makubaliano yalikuwa yamefikiwa.

Kocha wa zamani wa Ghana Ratomir Djukovic, kocha wa Botwana Peter Butler na kocha wa zamani wa Tanzania Kim Poulsen walikuwa miongoni mwa waliotarajia kupewa kazi hiyo lakini Kayiranga alisema kuwa walipendezwa na Constantine, na kwamba alikuwa tayari kujiunga na timu hiyo ya taifa la Rwanda.
Constantine aliye na leseni kutoka kwenye shirikisho la soka ulimwenguni majuzi aliisaidia Nea Salamis kutoka katika ligi ndogo ya Cypriot kufuzu kucheza katika ligi kuu. Constantine aliwahi pia kuwa mkufunzi wa mataifa ya Nepal, India, Malawi na Sudan.

Ferwafa inatarajia kukamilisha mipango hiyo wikendi hii nchini Tunisia wakati ambapo timu ya Taifa ya Rwanda itakuwa ikichuana na timu ya taifa ya Libya katika michuano ya kufuzu kwa mechi za mabingwa wa Afrika zitakazochezwa 2015. Kocha msaidizi bwana Cassa Andre Mbungo anatarajiwa kuiongoza timu hiyo wakati wa mchuano huo.

Ripoti katika wavuti wa Ferwafa zinaongezea kuwa kuna machache ambayo wanpaswa kuzungumzwa na Constantine kabla ya kumtangaza rasmi kama mkufunzi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa