Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YASAWAZISHA MBILI ZA YANGA.

Klabu ya Simba imezidi kujiimarisha kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara baada ya kusajili vifaa vipya viwili, Awadh Issa, kutoka Mtibwa Sugar ya Manungu, Morogoro na Ally Badru aliyekuwa anaichezea Canal Suez ya Misri, hivyo inakuwa kama imesawazisha baada ya watani zao kusajili wachezaji wawili pia.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema wachezaji hao kila mmoja amesaini mkataba wa miaka miwili na wanaamini uwapo wao utasaidia kukiimarisha kikosi chao ambacho kimemaliza mzunguko wa kwanza kikiwa katika nafasi ya nne.

Mtawala alisema tayari klabu yao iko katika mazungumzo na timu nyingine za Ligi Kuu ya Bara ili kuwahamishia wachezaji wengine kwa mkopo.

"Tuna nafasi moja lakini hilo si tatizo, kuna vijana wetu ambao bado wanahitaji uzoefu na kwetu Simba wamekosa nafasi ingawa ni wazuri, tutawapeleka kwa mkopo katika baadhi ya timu ambazo zimeonyesha nia ya kuwatumia," alieleza Mtawala.


Alisema Kamati ya Utendaji ya timu hiyo bado haijapanga kukutana lakini imeshaanza kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na Kocha Mkuu, Abdallah Kibaden 'King' katika ripoti yake.

Katibu huyo aliwataka mashabiki wa Simba kuwa na subira na kuamini timu yao itafanya vizuri katika mzunguko wa lala salama na kwamba tofauti ya pointi walizonazo dhidi ya watani zao si kubwa.

Badru na Issa pia ni wachezaji wa timu ya soka Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) na jana mchana baada ya kumaliza kusaini mikataba ya kuichezea Simba mbele ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, walirejea visiwani humo kuendelea na maandalizi ya mashindano ya Kombe la Chalenji.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe