Ruka hadi kwenye maudhui makuu

P-SQUARE KUWASHA MOTO DAR LEO.

Mapacha Peter na Paul Okoye wanaounda kundi la wanamuziki wawili la P-Square la Nigeria wameahidi kutoa shoo kali kwa mashabiki katika onyesho la leo kwenye viwanja vya Leaders Club, jijini, ikiwemo kutumbuiza kwa saa mbili mfululizo bila kupumzika.

Kundi la P-Squere ambalo linatikisa ulimwengu kwa singo ya 'Pesonaly', limekuja nchini kwa mwaliko wa kituo cha televisheni cha EATV na East Africa Redio; chini ya udhamini mkuu wa Vodacom na kapmuni za Hennessy na Mastermind.

Katika onyesho hilo, P-Square watasindikizwa na Lady Jaydee, Prof Jay, Jo Makini na Ben Pol ambao wote kwa pamoja jana waliahidi kutoa burudani ya kiwango cha juu katika kuchuana na wageni hao.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Peter alisema wamekuja nchini kutoa "shoo kali kwa mashabiki wa muziki na Watanzania wote kwa ujumla."

P-Square wanathamini muziki wa Afrika na ndio maana wanajitahidi kila siku kupiga staili ya kiafrika, alisema Peter, kwa ajili ya kuendeleza muziki kwa Bara la Afrika.

"Tunataka kuendeleza muziki wa Afrika kwa hiyo wasanii wa Tanzania tushirikiane pamoja," alisema Peter.

Alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha wanatoa burudani kabambe ya saa mbili mfululizo bila kupumnzika.

Naye Paul alisema wamefurahishwa na mapokezi ya Watanzania na ukarimu walioonyeshwa tangu wawasili "katika nchi (hii) ya kitalii" juzi usiku.

Alisema katika kulipa fadhila, P-Square itatoa burudani ambayo ni ya kwanza ya aina yake na ya funga mwaka 2013.

Aidha, aliwataka wanamuziki nchini kushirikiana pamoja ili kuhakikisha wanapeleka mbele muziki wa bara la Afrika.

"Sisi ni wamoja, tufanye kazi pamoja ili tukuze muziki wa Afrika kama ilivyo mabara mengine," alisema Paul.

Mkuu wa vipindi wa EATV Nasser Kingo alisema televisheni hiyo imejiandaa vizuri kwa onyesho hilo na kwamba usalama kwa mashabiki na ulinzi wa mali zao vitakuwepo vya kutosha.

Naye mkuu wa masoko na mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twisa alisema wameamua kushirikiana na EATV na East Africa Radio ili kutoa nafasi kwa wanamuziki wa Tanzania kujifunza kutoka kwa Wanigeria hao.

"Hakuna asiyewafahamu P-Square walivyoitoa kimasomaso Afrika katika muziki," alisema Twisa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe