Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MUME WA MAREHEMU NYAWANA YAMKUTA MAKUBWA.

Kaisi Musa Kaisi (Pichani) mume wa marehemu Nyawana ambaye alikuwa akitamba kwenye muziki wa taarabu hapa nchini hatimaye yamemkuta makubwa baada ya kutoswa na kundi la wanasalamu wenzake ambao kwa sasa wana umoja wao unaofahamika kwa jina la Umoja wa Wanasalamu mkoa wa Dar es Salaam na Pwani.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari hizi ambacho ni rafiki wa karibu na Kaisi Musa Kaisi ambaye ni mmoja kati ya wanasalamu maarufu hapa nchini kupitia vituo vya redio pamoja na magazeti alijikuta akitengwa na wenzake katika msiba wa marehemu mke wake aliyefariki kwa kuugua malaria.

Taarifa kamili zinasema kuwa Kaisi amekuwa na tabia ya kutoudhuria misiba ya wanasalamu wenzake huku ikidaiwa umaarufu ndio umemfanya ajione staa, chanzo chetu kiliendelea kusema kuwa wanasalamu wamekuwa na utaratibu mzuri wa kuudhuria misiba ya wadau wao hata kama si maarufu.

Kupitia afisa wao wa habari Salum Mfunga 'Rais wa mafukara Tz' amethibitisha habari hizo kuwa wanasalamu kwa pamoja wameamua kuachana kabisa na Kaisi na waliudhuria msiba wa Nyawana kwa sababu marehemu kabla ya kufikwa na mauti alikuwa mtangazaji katika kituo cha redio Passion.

'Ni kweli marehemu alikuwa mtangazaji Passion hivyo sisi kama wadau tuliamua kumsindikiza ndugu yetu huyo, kuhusu Kaisi kusema kweli hatuna habari naye kwani si mwenzetu tena, alianza kututenga tangia mwanzo hivyo kama umoja umeamua kuachana naye', alisema na kuongeza.


Mfunga ambaye anakubalika kwa hamasa zake amedai umoja wa wanasalamu uliikabidhi familia rambirambi yao ambapo mchango wa wanasalamu uliwezesha kupatikana kwa shilingi Laki moja na elfu Ishiriini (120,0000).

Fedha hizo alikabidhiwa mtoto mkubwa wa marehemu Nyawana na kumtosa mume wa marehemu Kaisi Musa Kaisi ambaye alionekana kuwa na huzuni, pia Kaisi Musa Kaisi inasemekana alijenga uhusiano wa kimapenzi kabla ya kufunga ndoa na marehemu Nyawana alipokuwa meneja wa kundi la taarabu la T-Moto huku ikidaiwa kuikacha ndoa yake ya awali na mkewe aliyezaa naye watoto.

Katika maisha yao mapya kati ya Kaisi na Nyawana hawajawahi kupata mtoto licha ya kila mmoja kuwa na watoto wawili nje ya ndoa yao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe