Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MESSI AJA NA MAAJABU MAPYA.

Lionel Messi atafanya kila awezalo kuhakikisha anapona jeraha la misuli ya paja ambalo alipata Jumapili na ambalo litamfanya akae nje ya soka kwa kati ya wiki sita na nane, mchezaji huyo wa Argentina ambaye pia ndiye Mchezaji Bora wa Mwaka Duniani alisema Jumanne.

Hayo ndiyo matamshi yake ya kwanza hadharani tangu aondoke kwenye mechi mapema wakati wa ushindi wa Barca wa 4-1 katika Real Betis. Messi alisema lengo lake kuu ni kurejea mchezoni mapema iwezekanavyo na kusaidia mabingwa hao wa Uhispania katika kutafuta kikombe.

"Kama wengi wenu mjuavyo, wiki chache zijazo, nitakuwa nikifanya kila liwezekanalo nipone jeraha nililopata majuzi,” Messi alisema kwenye ukurasa wake wa Facebook.

"Kwangu, ni masikitiko kwamba sitaweza kuchezea timu yangu kwa sasa,” akasema mchezaji huyo wa umri wa miaka 26.

"Kwa sasa, la muhimu zaidi ni kupata nafuu vyema ili niweze kusaidia wachezaji wenzangu na kuwazawadi nyote kwa uungaji mkono ambao mmneipa kwa njia bora zaidi niwezayo, kucheza soka.”

Messi aliondolewa kwenye mechi dakika ya 19 Seville baada yake kukimbia akishindania mpira na wapinzani.


Hilo lilikuwa jeraha lake la tatu kwenye paja baada ya matatizo sawa karibu na mwisho wa msimu uliopita.

Kutokuwepo kwake si kubaya kama vile wengi wanaweza kudhani kwani kuna uwezekano kwamba atarejea kabla ya Barca kukabiliana na wapinzani wao wa kupigania taji Atletico Madrid mwezi Januari na tayari wamefuzu kwa timu 16 bora katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Fowadi wa Brazil Neymar, aliyejiunga nao kutoka Santos kipindi cha kuhama wachezaji ni mchezaji mwenye uwezo wa kuwafaa sana Barca na mchezaji huyo wa umri wa miaka 21 anatarajiwa kuonyesha sababu yake kununuliwa euro 57 milioni ($76.6 milioni) wakati Messi atakuwa nje.

Raia huyo wa Argentina atakosa mechi mbili za mwisho za Barca katika dimba hilo kuu la Ulaya, dhidi ya Ajax Amsterdam na Celtic.

Pia hatacheza mechi za La Liga dhidi ya Granada, Athletic Bilbao, Villarreal na Getafe na mechi mbili za nyumbani na marudiano katika King's Cup dhidi ya Cartagena lakini anafaa kuwa amerudi tayari kwa pambano la La Liga Atletico wikendi ya Januari 11-12.

Barca wanaongoza ligi wakiwa alama tatu mbele ya Atletico na sita mbele ya wapinzani wao wa jadi Real Madrid walio wa tatu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe