Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JANJA YA RAGE YABAINIKA, YADAIWA ANATUMIA MASHABIKI WA YANGA KUMLAKI.

Imefahamika kwamba mwenyekiti wa Simba ambaye hivi karibuni alisimamishwa na kamati ya utendaji Ismail Aden Rage, inasemekana amekuwa akitumia ujanja wakati wa mapokezi yake na kulakiwa na watu wengi wanaokwenda na vuvuela huku wakimbeba juu juu.

Sasa imebainika kuwa mwenyekiti huyo wa Simba anatgumia kundi la mamluki ambao wengineo ni mashabiki wa kutupwa wa Yanga ambao hudiriki kuvaa jezi za Simba na kumuunga mkono, aidha ujanja huo umebainika na Simba wameandaa mpango rasmi wa kumng'oa Msimbazi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mjumbe mmoja wa kamati maalum ndani ta tawi moja maarufu jijini Dar es Salaam lkenye ushawishi mkubwa ndani ya klabu hiyo anasema kuwa ujanja wa Rage umejulikana hivi karibuni baada ya wapambe wake kuwakusanya mashabiki wa soka ambao wengine ni Yanga.


'Ni kweli Rage ametumia mashabiki wa soka na kujifanya wanampenda sana kisha kwenda uwanja wa ndege kumpokea, sisi wengine tunakaa nao na wengine ni marafiki zetu ambao tunawafahamu kama Yanga damu na wametuambia kuwa walialikwa na Rage ili kuwaonyesha Simba', alisema mumbe huyo.

Aidha amedai ili Simba imuondoe katika wadhifa huo ni lazima wajumbe wa kamati ya utendaji wachukue hatua nzito na kukubali kujitoa mhanga, amesema njia pekee ya kumuondoa Rage ni wajumbe wa kamati ya utendaji wote kwa pamoja wajizuru nyadhifa zao ili Rage ashindwe kuwa mwenyekiti kamili.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe