Ruka hadi kwenye maudhui makuu

IVO MAPUNDA ATEMWA GOR MAHIA

Tetesi za kutua kwa kipa wa zamani wa Moro United, Prisons na Yanga Ivo Mapunda ambaye anaichezea Gor Mahia ya Kenya katika klabu ya Simba huenda zikatimia baada ya kipa huyo kutokuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya Kenya.

Ivo Mapunda anatajwa kuwemo katika kikosi cha Simba kinachojiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Tanzania bara, taarifa zilizothibitishwa na chanzo chetu cha habari zinasema kuwa kipa huyo mzoefu aliyeitwa kwenye timu ya taifa, Taifa Stars inayojiandaa kucheza na Zimbabwe kesho hatoongezewa mkataba mwingine na Gor Mahia.

Kwa sasa Ivo anasugua benchi kama kipa namba mbili hivyo uongozi wa Gor Mahia umeamua kutomuongezea mkataba mwingine mchezaji huyo badala ya huu wa mwanzokumalizika rasmi, Ivo ameiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa Kenya lakini amejikuta katika wakati mgumu hasa anapoanzia benchi.

Kulingana na taarifa hiyo inaweka wazi nafasi yake kubwa kutua kwenye ligi kuu ya bara na Simba inatajwa kama timu pekee inayoweza kumsajili, lakini mtandao huu ulipoamua kumtafuta kipa huyo na kuzungumzia mikakati yake kama ataendelea kukipiga na Gor Mahia kwa mara nyingine.

Ivo amesema yeye kama mchezaji na kazi yake ni mpira hivyo timu yoyote ile ikiwa tayari kumsajili atakuwa radhi kwenda, anadai mkataba wakena Gor umemalizika hivyo milango iko wazi kwa timu yoyote inayomtaka imsajili.


Amedai yeye bado hajafanya mazungumzo yoyote na Simba wala timu nyingine ila meonyesha kuwa yuo tayari kuzungumza nao kwa vile mkataba wake na waajili wake umemalizika, hata hivyo Simba imeonyesha nia ya kumsajili kipa huyo kufuatia ripoti ya benchi la ufundi kuhitaji kipa, beki yakati, kiungo na mshambuliaji.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe