Ruka hadi kwenye maudhui makuu

GERRARD AMPUUZA FERGUSON.

Nahodha wa Uingereza Steven Gerrard amepuuzilia mbali madai ya meneja wa zamani wa Manchester United Alex Ferguson kwamba kiungo huyo wa kati wa Liverpool si “mchezaji nyota.”

Ferguson alitoa madai hayo kwenye tawasifu yake, ambayo ilichapishwa mwezi uliopita, lakini Gerrard anasema majaribio ya raia huyo wa Scotland ya kutaka kumnunua ni thibitisho tosha kwamba alithamini sana uwezo wake.

“Sikizeni, ana haki ya kuwa na maoni yake,” Gerrard aliambia jarida la Jumanne la gazeti la Uingereza la Daily Mail.

"Mimi ni shabiki wake; yeye ni mmoja wa mameneja bora zaidi duniani. Sipotezi usingizi kutokana na hilo. Katika maisha yangu ya soka, nimepokea pongezi kutoka kwa watu wa kila aina – yeye akiwa mmoja wao – na huwa nazipokea.

“Nimepokea pongezi za kushangaza kutoka kwake na alijaribu kuninununua, wakati mmoja. Labda hata mara mbili.

“Kwangu, la muhimu zaidi ni lile (meneja wa Liverpool) Brendan Rodgers na (meneja wa Uingereza) Roy Hodgson wanafikiria. Ninafikiri wamefurahishwa sana name na hilo tu ndilo laweza kunitia wasiwasi.


Gerrard, 33, anatarajiwa kuchezea Uingereza mechi yake ya 108 katika emchi za kirafiki dhidi ya Chile na Ujerumani, hatua itakayomfikisha kiwango sawa na nahodha aliyeshinda Kombe la Dunia 1966 Bobby Moore.

"Kuchezea taifa mechi 107 si jambo mbaya kwa mtu ambaye si nyota, si ndivyo?” akaongeza.

“Sikutarajia kucheza mechi nyingi kiasi hiki. Nilipocheza mechi yangu ya kwanza, nilijiwekea lengo la mechi 50 na kufunga mabao 10 kama ningeweza. Kwa hivyo kupata mechi 107 ni jambo ambalo najivunia sana, hasa kuungana na wachezaji wasifika.”

Rodgers alidai wiki iliyopita kwamba Gerrard huenda astaafu baada ya Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka ujao, lakini mchezaji huyo alisema kwa sasa hataki kufikiria kuhusu yajayo.

“Kwangu lengo langu ni: naweza kusaidia timu yangu ifike robofainali?” alisema.

“Sijafikiria sana kuhusu nini nitafanya baada ya Kombe la Dunia. Nafikiria tu kwenda na kujivunia Kombe la Dunia. Litakuwa jambo la kusisimua kuwa Brazil.

"Nina furaha sana kuwa nilisaidia timu yangu kufika huko, ni ufanisi mkubwa. Kwa sasa, mtazamo wetu unafaa kubadilika na kuwa: tunaweza kufanya nini tukifika huko?”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe