Ruka hadi kwenye maudhui makuu

FILAMU YA SIMBA YAZIDI KUNOGA: MZEE KINESI, HANSPOPE NAO WASIMAMISHWA.

MWENYEKITI aliyesimamishwa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage atarejea nchini Ijumaa na kulakiwa na mamia ya wanachama na ataitisha Mkutano Mkuu, ambao utafanyika Jumapili hii.

Na katika Mkutano huo, Rage amepanga kuwasimamisha Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji na baada ya hapo atasafiri kwenda nje ya nchi.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji waliobaki Simba SC ni Joseph Itang’are ‘Kinesi’, Said Pamba, Ibrahim Masoud ‘Maestro’, Swedi Nkwabi na Zacharia Hans Poppe.

Habari za kiuchunguzi, ambazo tumezipata zimesema kwamba, Rage amekwishawasiliana na wafuasi wake wa Dar es Salaam na wameandaa mapokezi makubwa kwake atakapokuwa anawasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Ijumaa.

Baada ya hapo, Rage ataitisha Mkutano Mkuu wa dharula Jumapili na siku hiyo atawasimamisha Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji.


“Ni kwamba tumekwishajipanga na Mwenyekiti anarudi hapa Ijumaa na Jumapili unafanyika Mkutano Mkuu, Kinesi na wenzake wote nje,”alisema mmoja wanachama wanaomuunga mkono Rage ambaye kwa sasa yuko nchini Sudan kwa shughuli zake za kisiasa.

Unaikumbuka hii? Mapema mwaka huu alisimamishwa na wanachama akiwa India na aliporejea alipokewa kifalme akaendelea kupeta.

Hatua hiyo inafuatia kikao cha Kamati ya Utendaji ya Simba kilichokutana juzi mjini Dar es Salaam na kufikia uamuzi wa kumsimamisha Rage ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Mjini kwa tiketi ya CCM, kwa kutokuwa na imani naye.

Rage anatuhumiwa kuchukua maamuzi mazito ya klabu bila kuwashirikisha wenzake na mengi yamekuwa yakiiweka klabu matatani. Pia, anatuhumiwa kwa ubadhirifu wa fedha za klabu na kukwamisha mambo mengi ya kimaendeleo ndani ya klabu, ikiwemo mabadiliko ya Katiba.

Baada ya kumsimamisha Rage, Kamati ya Utendaji pia ilimteua Joseph Itang’are ‘Kinesi’ kukaimu Uenyekiti wa klabu hadi hapo Mkutano Mkuu utakapofanyika.

Kinesi pia alikuwa anakaimu nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa klabu, iliyoachwa wazi na Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ aliyejiuzulu mapema mwaka huu, ambaye sasa ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Pamoja na kumsimamisha Rage, Kamati ya Utendaji pia imewasimamisha makocha wa kikosi cha kwanza, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ na Msaidizi wake, Jamhuri Mussa Kihwelo ‘Julio’.

Kamati imeamua kwa sasa timu itakuwa chini ya kocha wa timu ya vijana, Simba B, Suleiman Abdallah Matola ‘Veron’ ambaye atakuwa pia Msaidizi wa kocha Mkuu mpya wa kigeni, atakayetambulishwa Desemba 1, mwaka huu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe