Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CRISTIANO RONALDO AKARIBIA TUZO YA BALLON D'OR

KATIKA usiku ambao Cristiano Ronaldo alifunga mabao matatu matamu, hat-trick iliyoipeleka Ureno Fainali zijazo za Kombe la Dunia mwakani, FIFA imeongeza muda wa kupiga kura za kuchagua mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, Ballon d’Or.

Zoezi la upigaji kura lilifungwa Novemba 15, lakini Manahodha, Makocha Vyombo vya Habari ambavyo hazijawasilisha kura zao, wamepewa siku tisa zaidi kuwasilisha orodha zao za wachezaji watatu wa kwanza.

FIFA, ambayo imethibitisha uamuzi wake leo asubuhi, pia imethibitisha kwamba wale ambao tayari wamekwishapiga kura wanaweza kurekebisha majina yao na kuwasilisha tena.

Washindani: Nyota wa Barcelona, Lionel Messi (kushoto) amekwishashinda tuzo nne za Ballon d'Or na Franck Ribery wa Ufaransa na Bayern Munich (kulia) anapewa nafasi ya kufanya vizuri baada ya kushinda mataji matatu akiwa Bayern Munich.


Ronaldo jana usiku ameifungia Ureno mao matatu peke yake ikishinda 3-2 dhidi ya Sweden na kukata tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani Brazil.

Ureno inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mao 4-2 baada ya awali kushinda 1-0 wiki iliyopita nyumbani, bao pekee la Ronaldo. Zlatan Ibrahimovic alijitahidi kuisaidia timu yake jana na akafunga mabao mawili, lakini bahati haikuwa yao.

Ronaldo alifunga mabao yake katika dakika za 50, 77 na 79, wakati  Ibrahimovic alifunga dakika ya 68 na 72.


ORODHA KAMILI YA WACHEZAJI 23 WANAOWANIA TUZO YA MWANASOKA WA BORA WA DUNIA...

Gareth Bale (Wales/Real Madrid)
Edinson Cavani (Uruguay/PSG)
Cristiano Ronaldo (Ureno/Real Madrid)
Radamel Falcao (Colombia/Monaco)
Eden Hazard (Ubelgiji/Chelsea)
Zlatan Ibrahimovic (Sweden/PSG)
Andres Iniesta (Hispania/Barcelona)
Philipp Lahm (Ujerumani/Bayern Munich)
Robert Lewandowski (Poland/Dortmund)
Lionel Messi (Argentina/Barcelona)
Thomas Muller (Ujerumani/Bayern Munich)
Manuel Neuer (Ujerumani/Bayern Munich)
Neymar (Brazil/Barcelona)
Mesut Ozil (Ujerumani/Arsenal)
Andrea Pirlo (Italia/Juventus)
Franck Ribery (Ufaransa/Bayern Munich)
Arjen Robben (Uholanzi/Bayern Munich)
Bastian Schweinsteiger (Ujerumani/Bayern Munich)
Luis Suarez (Uruguay/Liverpool)
Thiago Silva (Brazil/PSG)
Yaya Toure (Ivory Coast/Manchester City)
Robin van Persie (Uholanzi/Manchester United)
Xavi (Hispania/Barcelona)

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe