Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ABEL DHAIRA ATEMWA RASMI SIMBA.

SIMBA SC inatafuta kipa mzuri wa kumsajili katika dirisha dogo, wakati huo huo inafikiria kuachana na kipa wake, Mganda, Abbel Dhaira ikibidi mapema iwezekanavyo au mwishoni mwa msimu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema leo kwamba, kutokana na kanuni mpya ya usajili wa wachezaji wa kigeni msimu ujao ya wachezaji watatu kutoka watano, hawatahitaji kipa mgeni.

Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), amesema kwamba kwa sababu hiyo lazima waachane na Dhaira mwishoni mwa msimu, au kama atapata timu hata sasa ambayo itakuwa tayari kuilipa Simba, watamuuza.

Poppe amesema kwa sasa Simba SC tayari inasaka kipa atakayekwenda kuwa pamoja na makipa wa wazawa, Abuu Hasimu na Andrew Ntalla.

“Niseme wazi, tunatafuta kipa. Huu ni mchakato makini sana na hatutaki kurudia kosa. Tunatafuta kipa mzawa, kwanza awe mwaminifu na mwenye uwezo mkubwa,”alisema.

Kuhusu habari kwamba, klabu hiyo inabadilisha benchi la Ufundi, Poppe amesema kwamba huo si ukweli kwa sababu hakuna kikao chochote kilichoketi kujadili suala hilo.


“Ripoti ya kocha (ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu) ndiyo kwanza inafika leo, wala hakuna kikao kilichoketi kuijadili, sasa hizo taarifa zinatoka wapi?”alihoji Poppe na kuongeza; “Sisi tunajua kuna hizo presha za kufukuza makocha, lakini hatujui haswa zinatoka wapi, mimi ninaomba nyinyi Waandishi muache kuvuruga wakati huu,”alisema.

Wakatu huo huo: Viongozi wa matawi yote Dar es Salaam wanatarajiwa wanatarajiwa kukutana makao makuu ya klabu Ijumaa asubuhi, kujadili marekebisho ya Katiba, mchakato unaoendelea vizuri hivi sasa klabu hiyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe