Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Viwanja vya bei nafuu Afrika Kaskazini, Yanga SC waige....


Kwa nini viwanja vya michezo ni vya gharama nafuu zaidi kujengwa katika nchi za Afrika Kaskazini?

Nilifanya utafiti na kugundua kuwa ujenzi wa viwanja vya michezo katika Afrika Kaskazini ni wa gharama nafuu zaidi ukilinganisha na ujenzi wa viwanja katika maeneo mengine ya Afrika.

Kwa mfano, ujenzi wa Uwanja wa Prince Moulay wenye uwezo wa kuchukua watu 65,000, ambao uliandaa Fainali ya AFCON 2025, uligharimu dola milioni 75 pekee, wakati viwanja vilivyoandaa fainali za AFCON za mwaka 2021 na 2023 nchini Cameroon na Côte d’Ivoire viligharimu zaidi ya dola milioni 200.

Mfano mwingine ni uwanja mpya wa Hoima City nchini Uganda, wenye uwezo wa watu 20,000, uliojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 484 za Uganda (sawa na dola milioni 131). Wakati huo huo, uwanja wenye uwezo wa watu 93,000 nchini Misri ulijengwa kwa gharama ya pauni milioni 900 za Misri (sawa na dola milioni 20).

Nataka tu kufahamu ni kwa nini ujenzi ni wa gharama nafuu zaidi Afrika Kaskazini. Je, ni kwamba viongozi wetu hawako waaminifu kwetu, au kuna sababu maalum zinazosababisha ujenzi wa viwanja kuwa nafuu zaidi Afrika Kaskazini ukilinganisha na maeneo mengine ya Afrika?


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa