Mwamba huyu hapa Tresor Mputu mabi anatajwa kuwa ndiye mchezaji bora wa muda wote wa TP Mazembe yaani sio Rainford Kalaba au Mbwana Samatta anayeheshimiwa zaidi pale Mazembe.
Imagine kuna kipindi mzee arsène wenger aliwahi kumuhita kucheza arsenal lakini mwamba alikataa akisema hali ya hewa ya England ni changamoto kwake.
Mputu alijiunga na TP Mazembe mwaka 2002 ambapo alicheza mechi 292 na kufunga magoli 144.
Ameshinda mataji yafuatayo akiwa na TP Mazembe;
1:Caf Champions mara 1 mwaka 2009
2:Caf Super Cup mara 1 mwaka 2010
3:Ligi Kuu ya Congo DRC mara 5
2006,2007,2009,2011 na 2012.
Tuzo binafsi alizoshinda Mputu ni
1:Mchezaji Bora kwa wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika mwaka 2009.
Mchezaji Bora Ligi Kuu ya DR Congo mara 3; 2007,2009 na 2011.
Tuzo ya mfungaji Bora IFFHS 2007.
Mputu amecheza vilabu viwili tu kwenye career yake ya mpira mwaka 2014 alijiunga na Kabuscorp ya Angola ambapo alicheza mechi 49 na kufunga goli 18 mwaka 2016 akarejea tena TP Mazembe.
Akiwa na jezi ya timu ya taifa ya Leopards, Mputu alicheza mechi 47 na kufunga goli 14.
Maisha yake nje ya uwanja yalikuwa ni ya majivuno sana mfano mashabiki zake walipotaka kumuona Mputu alikuwa hashushi kabisa vioo vya gari yake na hata kumngusa tu ni kosa kubwa.
Rais wa TP Mazembe alimjengea kiwanja chake binafsi cha mazoezi. Kwa ufupi Mputu alifaidi sana pesa za Moise Katumbi haswa.
Kwa ufupi yapo mengi yanayomuhusu Mputu. Next time nitakuletea story yakushindania ufalme kati ya Mputu na Mbwana Samatta ndani ya TP Mazembe.
