Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA WAANZE UPYA MCHAKATO WA MABADILIKO

Na Prince Hoza Matua

KWENYE hali ya kushangaza, Mwekezaji wa Klabu ya Simba, Mohamed Dewji kupitia ukurasa wake wa Instagram amehoji kwenye ukurasa wa Klabu ya Simba kuwa suala la Mabadiliko ndani ya Simba limefikia wapi?
.
Jambo ambalo limewashangaza wengi ni namna ambavyo Mwekezaji huyo amekuja kuuhoji uongozi wa Simba kuhusu suala la Mabadiliko ikiwa naye ni sehemu ya watu wanaohusika na kufanya Mabadiliko ndani ya Simba na huku ikiwa ni siku chache tangu zitoke tetesi za kwamba Bilionea huyo amejiondoa ndani ya Simba.
.
Mo Dewji anaahidi kuwaacha njiapanda mashabiki wa Klabu hiyo juu ya yeye kuwepo Simba na mbaya zaidi anahoji mitandaoni badala ya kuwafuata viongozi wenzake kwenye ofisi zao.

Kwa vyovyote mchakato wa mabadiliko ya klabu ya Simba SC inaonekana kama ya kiini macho na badala yake klabu ya Simba wanatakiwa kuanza upya mchakato, Wekundu hao wa Msimbazi, wameshindwa kukamilisha mchakato wa uwekezaji na kilichobaki ni sinema tu.

Kitendo cha MO Dewji kuhoji mchakato wa mabadiliko unakwendaje wakati na yeye ni sehemu ya viongozi, mchakato wa Simba unaonrkana kufeli kwani unapingana na matakwa ya serikali ambapo

Serikali inavitaka vilabu vya soka nchini vimavyotaka kuingia kwenye mabadiliko waakikishe wawekezaji wawe watatu na kuendelea na si mmoja kama ambavyo wanavyafanya Simba SC.

Mchakato wa mabadiliko wa klabu ya Simba unaendeshwa na mtu mmoja ambaye ni Mohamed Dewji "MO Dewji", Simba walitembea na mwekezaji mmoja aliyebahatika kubadili katiba ambayo inamfanya kuwa mmiliki na pia kuunda Bodi ya Wakurugenzi.

Pia mwekezaji MO Dewji, ameajiri CEO wa klabu halafu baadaye tunamsikia mwekezaji anaulizia mchakato wa mabadiliko kwa viongozi wa klahu, siyo siri mchakato wa mabadiliko wa Simba awamu ya kwanza imefeli na kinachopaswa kwa klabu hiyo ni kuanza mchakato upya.

Itakuwa vizuri sana endapo uongozi wa Simba wataanza upya mchakato huo wa mabadiliko na pia kubadili katiba ya klabu ambayo itampa nguvu mwenyekiti wa klabu hiyo Ili awe pia mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi.

Klabu inatakiwa kubaki na Hisa, asilimia 51 na zilizobaki asilimia 49 wapewe wawekezaji, MO Dewji anajua fika mchakato wa mabadiliko wa Simba unatakiwa kuanza upya na ndio maana amehoji.

Ule mchakato walioufanya hapo awali umegoma na serikali imeukataa ni bora waanze upya, nahisi viongozi wa Simba chini ya Murtaza Mangungu unafungua milango ya kuanza upya na ndio maana wameanza na suala la kuingiza wanachama wapya.

Uongozi wa Simba unapaswa kuwaiga Yanga katika suala la transformation, kwani Yanga walifanya mchakato wao bila kushawishiwa na GSM ambaye ndiye mfadhili kama ilivyo kwa MO Dewji.

Yanga waliamua kwenda Hispania kujifunza uwekezaji na wakaanza mchakato wao vizuri pasipo kulumbana, wanachama wa Yanga SC walifurahishwa na asilimia 51 ambazo wamepewa wanachama na pia kufurahishwa wawekezaji kupewa 49.

Bodi ya Wakurugenzi ya Yanga itaongozwa na Rais wa klabu, tofauti na ilivyo kwa Simba ambapo mwenyekiti wa klabu anageuka kama mwanachama wa kawaida ambaye hajui chochote kuhusu maendeleo ya klabu yake.

Simba inatia huruma pale mwenyekiti wa klabu yake anaposhambuliwa na mashabiki wakishinikiza ajiuzuru, mashabiki hao waliomshambulia mwenyekiti wa Simba wanadai ni yeye ni tatizo kwa Simba kutofanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa.

Lakini kama wangeujua ukweli wasingejaribu hata kidogo kumshambulia kwa sababu mwenyekiti wa Simba ni kama wao tu hajui chochote, viongozi wa Bodi ya Wakurugenzi inayoongozwa na MO Dewji ndio inayotekeleza yote ya Simba katika suala la kufanya usajili na maandalizi ya timu na siyo mwenyekiti wa klabu.

ALAMSIKI


 


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa