Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Nani yupo nyuma ya mpango wa Mangungu kushambuliwa?

Anaandika Mdau

Dhahiri fujo alizofanyiwa Mwenyekiti wa klabu ya Simba Murtaza Mangungu ni mpango uliofeli ambao umeratibiwa kishamba, swali ni nani aliyepo nyuma ya huu USHAMBA?

Dhahiri kuna mashabiki wameandaliwa kumfanyia fujo Mwenyekiti wa klabu bila sababu ya msingi. Manake kama wangekuwa na hasira na viongozi kwanini Cresentius Magori Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu hakufanyiwa fujo ilihali nayeye alikuwepo Taifa na akatoka kama mfalme?

Bodi ya Wakurugenzi ya Simba ndiyo KILA KITU katika kuiongoza klabu kwa sasa kwa mujibu wa makubaliano ya upande wa wanachama na upande wa MO na Mwenyekiti wake ameteuliwa na MO.

Mwenyekiti wa Klabu ambaye anatokana na wanachama HANA LOLOTE mbele ya Mwenyekiti wa Bodi, kama kweli mashabiki wana hasira na viongozi kwanini wambague Mwenyekiti wa Bodi na yule wa Wanachama? Wangeshambuliwa wote kuonyesha hasira zao kwa uongozi, lakini hili lilifanyika ni Ushamba ulioratibiwa Kishamba na wajinga ambao hawana wanalojua, waliotekeleza ni wapuuzi ambao wametumika kama TOILET PAPER tu.

Kuna watu wanajidanganya kwamba Mangungu atatolewa kwa vurugu ili wafanya wanachotaka, wasahau kwakuwa ishu sio Mangungu, Serikali ndiyo iliyotoa maagizo ya marekebisho ya Katiba ili klabu ijiendeshe, najua hapa ndipo kuna MZIZI WA TATIZO hawa vijana wanatumika tu.

Sasa upande wa Mangungu ukipanga vijana kushambulia Mwenyekiti wa Bodi itakuaje? Punguzeni ushamba hizi mambo za kizamani sana na nyakati hizi haziwezi kufanya kazi.

Timu lenu lina alama 1 na haliwezi kwenda popote, NBC PL ina “wenyewe” tayari na washakaa pahala pao, nyinyi mnatengenezeana watu wa kufanya vurugu, ujinga kiasi gani. Mnadhani eti Mangungu ndo ataonekana tatizo ili mtu au watu fulani waonekane wazuri, upuuzi.

Subirini mkutane nao GONGOWAZI wakuchapeni tena halafu ubingwa mkose, muone kama hawa mnaowatuma hawajawageuka.

Murtaza Mangungu

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa