Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Moallin kurejea tena nchini

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Yanga, Abdihamid Moallin ‘Master Lecturer’, huenda akarejea Tanzania hivi karibuni ikiwa atafikia makubaliano na timu tatu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara, baada ya kuonyesha uhitaji mkubwa kwa kocha huyo.

Kocha huyo mwenye uraia wa Marekani akiwa na asili ya Somalia, kwa sasa yupo mapumziko Marekani tangu alipoachana na Yanga Julai 27, 2025, akiwa ni Mkurugenzi wa Ufundi, ingawa huenda muda wowote akarejea nchini ikiwa mazungumzo na timu hizo yatafikiwa ipasavyo.

Hata hivyo, Mwanaspoti limepenyezewa taarifa zikieleza miongoni mwa timu zinazofanya mazungumzo na Moallin, kimya kimya ni TRA United inayonolewa na Mrundi Etienne Ndayiragije, ambaye hadi sasa kumekuwa na sintofahamu juu ya kibarua chake.

Ndayiragije aliyejiunga na timu hiyo baada ya kuachana na Kenya Police FC ya Kenya, Oktoba 29, 2025, baada ya kuipa pia ubingwa wa Ligi ya Kenya, inadaiwa hana uhusiano mzuri na mabosi wa TRA, jambo linalofungua mazungumzo hayo na Moallin.

Kocha huyo aliipa Kenya Police ubingwa huo ukiwa ni wa kwanza kwa kikosi hicho katika historia tangu kilipopanda daraja mwaka 2021, hivyo, kuzima utawala wa Gor Mahia iliyochukua mara mbili mfululizo kuanzia msimu wa 2022-2023 na 2023-2024.

Moallin aliyewahi kuifundisha Azam FC na KMC, inaelezwa anafanya mazungumzo na timu tatu za Tanzania, ambazo hata hivyo, Mwanaspoti linafahamu TRA United ni miongoni mwao, licha ya usiri uliotawala wa kutotaka kuweka wazi nyingine kwa sasa.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa