Na Abdul Makambo
0787905328.
JINA la Juma Said Nyoso si geni kwa wapenda soka hapa nchini pi ni jina maarufu katika masuala haya ya mchezo wa soka.
Nyoso ni beki au mlinzi wa kati akizimudu namba 4 na 5, miaka ya katikati ya miaka ya 2000 aliibukia kwenye Ligi Kuu bara akiwa kwenye klabu ya Ashanti ya Ilala jijini Dar es Salaam.
Akiwa Ashanti ndipo alipoonekana na kocha wa timu ya taifa, Taifa Stars miaka ile Mbrazil Marcio Maximo na kumuita kwenye kikosi cha National team.
Nyoso ni beki makini wa kati na ana ball control na mtulivu wakati
mwingine anacheza soka la kistaarabu kutegemea na mechi lakini kama mechi kubwa kubwa anakua ni mtu hatari na asiependa masihara kiwanjani.
Kuna kipindi fulani akiwa Simba alikua pacha wake ni Kelvin Yondan "Vidic"' na hata kwenye timu ya taifa, Taifa Stars pia alikua anasimama na Yondan.
Washambuliaji wengi hapa nchini wamekua wanamhofia Nyoso, hata John Bocco na Meddy Kagere walikua wanapata wakati mgumu wakikutana na Nyoso.
Hata kuna wakati fulani Yanga ikicheza na timu ya Mbeya City mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele alikua anakabwa na kusukumwa halafu alikua hamuangalii usoni zote ni mbinu za kimchezo mshambuliaji akuogope.
Nyoso alikua ni beki mwenye mikwala kiwanjani alikua anafuata nyayo za mabeki wa zamani kama Omary Chogo na Mohamed Kajole wa Simba na Omary Kapera, Athumani Kilambo na Salum Kabunda wa Yanga.
Bila shaka wasomaji wa Mambo Uwanjani Blog mumemfahamu Juma Said Nyoso.beki wa zamani wa kimataifa wa Tanzania ambaye hatosahaulika kwa matukio yake ikiwemo la kunshika makalioni mshambuliaji wa Simba na Azam FC, John Bocco ambalo lilipelekea mpaka kufungiwa na Bodi ya Ligi, TPLB.


