Nimewafuatilia GSM na Mo ni matajiri wakubwa Tanzania, wote wana mchango mkubwa sana kwa timu zao
Huwezi kutaja maendeleo ya Yanga bila GSM huwezi kutaja maendeleo ya Simba bila Mo
Kinachoifanya Yanga kutamba sa hivi ni busara za GSM anajua mipaka yake na anaijua kazi yake vizuri sana
Sijawahi kumuona akitoa tamko lolote au kuingilia jambo lolote pale Yanga sababu kuna mtu wake anamuamini ambaye ni Eng Hersi
Njoo kwa Mo sasa suala la kuingilia utendaji wa timu na kutoa matamko yanayo zua taharuki kwake ni kitu cha kawaida
Tajiri Mo kuna muda aliandika tamko la kususa hadharani, kuna muda pia aliandika tamko kusema kuwa kufungwa goli tano na yanga kuna wachezaji wana hujumu timu bila kuwa na ushahidi wowote, tajiri mo kuna muda aliandika hadharani kuwa simba inahitaji kipa mpya na akamsajili na sijui kipa wake aliishia wapi, juzi hapa kaandika kuulizia mabadiliko ya simba wakati anajua kila kitu kuhusu simba.
Shida ya watu wengi wanafikiri mtu kuwa tajiri ndo kujua kila kitu matokeo yake mo anaweza fanya kitu chochote na watu wakachukulia kitu cha kawaida ila ukiangalia kwa undani kuna madhara yake kuliko faida
Nafikiri ni wakati sasa mo ajifunze kwa gsm aache watu wa mpira wafanye kazi yao bila kuwaingilia bila kutoa matamko yanayoweza kuigawa timu ambayo hayana faida yoyote kwa timu
Nafikiri mashabiki uchwara waliokwenda kumshambulia mangungu wangeenda kumshauri mo kuwa ajifunze kwa GSM
